Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto atoa ushahidi alikubali kukutana na Rais Uhuru kumaliza uhasama

159decfb25d5180f DP Ruto atoa ushahidi alikubali kukutana na Rais Uhuru kumaliza uhasama

Sun, 3 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Ruto amechapisha barua aliyotumia muungano wa maaskofu akikubali wito wao kumpatanisha na Rais Uhuru.

Amesema yeye yuko tayari na bila masharti yoyote kuketi na Uhuru kwenye meza yao ili kuhakikisha kuwa taifa linaendelea kwa usalama.

Gazeti la humu nchini Jumapili lilisema kambi za Ruto na Uhuru zilikosa kuonyesha haja ya wawili hao kuketi kumaliza uhasama baina yaoNaibu Rais William Ruto ametoa ushahidi kupinga madai kuwa upande wake umekuwa kziingiti katika juhudi za kumpatanisha na Rais Uhuru Kenyatta.

Ruto alitoa ushahidi wake kuonyesha alikubali wito wa maaskofu wa kanisa katoliki kumpatanisha na Rais.

Gazeti la humu nchini lilichapisha taarifa likisema kambi za Ruto na Uhuru zimekuwa na kiburi hazitaki maridhiano.

Hata hivyo, kupitia kurasa zake mtandaoni Ruto alichapisha barua aliyotumia muungano wa maaskofu akisema yeye yuko tayari kuketi kwenye meza moja na Uhuru.

"Ninashukuru sana na kukubali kwa unyenyekevu kuwa uhusiano wangu na Rais umekuwa suala la kuwapa wasiwasi kuhusiana na umoja humu nchini. Nataka niwahakikishia kuwa mimi sina lolote kumhusu Rais," DP alisema kwenye barua hiyo.

Ruto alisema amekuwa akimuunga Kenyatta mkono kisiasa kuanzia 2013 na hakufanya hivyo na masharti yoyote.

"Nilimuunga mkono bila masharti na ninaheshimu wajibu wake kama rais wa taifa. Ninaheshimu pia uamuzi wa Rais kufanyia serikali yake mabadiliko ili kuwa namna anayoamini itatekeleza sera zake," alisema DP kwenye barua hiyo.

Muheria aliambia gazeti la Sunday Nation kuwa kilichobaki kwao ni maombi sasa ili wawili hao waguswe nyoyo na kukubali kumaliza uhasama.

"Tunaendelea kuomba ili mwaliko wetu ufanyike," Muheria aliambia gazeti hilo kuhusu juhudi za kanisa kupatanisha wakuu hao wa serikali ya Jubilee.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke