Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto atamuonyesha kivumbi Raila 2022, Farah Maalim asema

0fgjhs6gk6ppoalsd DP Ruto atamuonyesha kivumbi Raila 2022, Farah Maalim asema

Tue, 27 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Aliyekuwa naibu spika wa bunge Farah Maalim amedai kwamba Naibu Rais William Ruto ana wafuasi wengi kumliko kinara wa chama cha ODM Raila OdingaMaalim alisema iwapo kinyang'anyiro cha urais 2022 kitakuwa kati ya vigogo hao wawili, basi Ruto ataibuka mshindi bila pingamizi lolote Raila na Ruto ni mahasidi wakubwa wa kisiasi na wote wanaazimia kuwania urais ila Raila hajatangaza rasmi mpango wake wa 2022Aliyekuwa naibu spika wa bunge Farah Maalimu amedai kwamba Naibu Rais William Ruto atashinda uchaguzi mkuu wa 2022 kabla ya saa nne asubuhi iwapo atamenyama na kinara wa chama cha ODM Raila Odinga.

Maalim ameyasema hayo huku siasa za kumrithi Rais Uhuru Kenyatta zikipamba moto nchini ikiwa imesalia mwaka mmoja uchaguzi mkuu ufike.



Read also

Mpango Wangu ni Kumshinda DP Ruto Mwaka Ujao, Kalonzo Asema

Akizungumza na runinga ya TV47 Jumatatu, Julai 26, Maalim alisema ingawa hampendi Ruto na hawezi akampigia kura, ana imani kwamba ataibuka mshindi wa uchaguzi wa urais akiwa kinyang'anyironi pekee na Raila.

" Kama Raila na Ruto ndio watakuwa debeni pekee 2022, amini usiamini Ruto ataibuka mshindi kabla ya saa nne asubuhi, mimi kivyangu simpendi Ruto na siwezi nikampigia kura" Maalim alisema.

Huku uchaguzi mkuu ukikaribia, kinara wa chama cha ODM Raila Odinga bado hajatangaza wazi iwapo atawania kiti cha urais lakini kumekuwa na fununu kutoka kwa baadhi ya viongozi ndani ya chama chake kwamba atakuwa debeni.

Mwenyekiti wa chama hicho John Mbadi alikuwa ametangaza awali kwamba Raila atakuwa miongoni mwa wawaniaji wa kiti cha urais.

Ruto tayari ametangaza kuwania urais kwa tiketi ya chama chake kipya cha UDA ingawa bado hajaondoka rasmi katika chama cha Jubilee ambapo pia anashikilia nafasi ya naibu kiongozi.



Read also

Kitu Ilikuwa Safi: Tume ya IEBC Yasema Kuhusu Uchaguzi wa Kiambaa

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke