Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto ataingia Ikulu, mchanganuzi wa kisiasa Makau Mutua asema

C893b905d77b021a DP Ruto ataingia Ikulu, mchanganuzi wa kisiasa Makau Mutua asema

Sun, 4 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Makau amesema DP amekuwa akijijenga kisiasa huku wapinzani wake wakijikokota na kutapatapaAlisema hilo likiendelea DP ataingia Ikulu asubuhi na mapema siku ya kupiga kura ya urais 2022Makau amekuwa mmoja wa wakosoaji wa DP na makala yake ya Jumapili yaliwashangaza wengiMchanganuzi wa kisiasa Makau Mutua amewashangaza wengi kutokana na makala yake kwenye gazeti la Nation Jumapili Julai 4.

Makau, ambaye amekuwa mmoja wa wakosoaji wakuu wa Naibu Rais William Ruto, alisema amelazimika kukiri kuwa kuna dalili za DP kuingia Ikulu.

Alisema hilo linachangiwa pakubwa na wapinzani wa DP ambao wamekosa mikakati ya safari yao kuingia Ikulu.

"Uchanganuzi wangu unaniambia kuwa kuna nafasi kubwa kwa DP William Ruto, jamaa ambaye aliponea makali ya mahakama ya ICC kwa tundu la sindano, huenda akawa rais wa tano wa Jamhuri ya Kenya," aliandika Makau kwenye makala hayo.

Alisema DP anaendelea kujitafutia umaarufu kila uchao huku wenzake kwenye muungano wa One Kenya Alliance wakiwa usingizini.

"Ruto anaendelea kuvuma wakati ambapo wapinzani wake wanaendelea kujikokota. Wamekuwa ndio watermelons. Ndio maanaka ninatabiri kuwa ifikapo siku ya uchaguzi 2022, Ruto ataingia Ikulu asubuhi na mapema," aliendelea kuandika.

Alisema mbinu ya DP kuwa mkarimu kwa wanasiasa imemuwezesha kuwa na ushawishi mkubwa kwao.



Hata hivyo, Makau alionya wandani wa DP kuwa hawa lolote la kusherekea kwa sasa kwa sababu uchaguzi ungali mbali.

Alisema amekuwepo wakati ambapo mambo katika ulingo wa siasa yalibadilika kwa siku chache na hivyo lolote lawezekana kabla ya 2022.

Vigogo Kalonzo Musyoka, Moses Wetangula, Raila Odinga na Musalia Mudavadi wamekuwa wakitapatapa kila uchao bila kutangaza msimamo kamili kuhusu nia yao 2022.

Raila hata hivyo alionya kuwa Tsunami ya kisiasa inajiri na itamsomba DP Ruto na wandani wake katika safari ya kuingia Ikulu.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke