Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto ashtumiwa kwa unafiki

366c42309d36b5ae DP Ruto ashtumiwa kwa unafiki

Thu, 16 Dec 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kabogo alisema DP Ruto ni kiongozi mnafiki sana na hawezi kukubaliana naye kwenye suala la kuvunjwa kwa vyamaAliwataka wakazi wa Mt Kenya kutounga mkono vyama vya Ruto na Raila katika nyadhifa za ubunge na ugavanaAlitabiri kuwa Ruto na Raila wataungana baada ya uchaguzi mkuu ujao huku akionya eneo la Mt Kenya kuwa litaachwa kinywa waziAliyekuwa gavana wa Kiambu William Kabogo amemtaka naibu rais William Ruto kama kiongozi mnafiki sana.

Akiongea kwenye mahojiano na runinga ya Inooro, Kabogo alisema amekuwa akitengamana na viongozi kadhaa lakini hakuna aliye kama Ruto.

Alikosoa DP kwa kuwataka viongozi wengine kuvunja vyao ili kuingia kwenye chama chake cha United Democratic Alliance.

“KWacha nikuambie ukweli. Hakuna mtu mnafiki hii dunia kama yeye. Na ndio maana mimi alikuja kwangu na hatukuskizana. Huwezi kuniambia nivunje vyama vyetu. Na Yeye akienda ngome yake anaambia watu wake wasiingie vyama vya wengine,

Kwani ni nini hii ametupangia? Amekuwa akisemakuwa serikali yake na Uhuru Kenyatta ilifanya kazi vizuri 2013 hadi 2017. Wakati huo ilikuwa ni TNA na URP, kwa nini saa hii tusiwe na vyama vyetu?” alisema Kabogo

Read also

Oparanya: Nitafikisha Viti Vingi Ajabu Eneo Magharibi kwa Kapu la Azimio

Alisema eneo la Mt Kenya linafaa kuwa makini kwani huenda wakabaki bila mtetezi kisiasa iwapo wataingia vyama vya Ruto au Raila Odinga.

“Mtapigia kura Raila au Ruto kuwa rais, na kisha mwapee viti vya ubunge. Siri ni mwapigie kura ya urais lakini msiwape viti vya ubunge. Kwa sababu hiyo ndio itatusaidia, hawa watu ni wale wale,” alisema Kabogo.

Kabogo alikosoa ahadi za Ruto na Raila akisema kile wanafanya ni kuhadaa tu wapiga kura ili kuwashawishi kwa ajili ya 2022.

“Najiuliza aje mama mboga atapewa kiti ya DO au gani ndio serikali iwe yake? Mwingine anakuambia eti atakuletea KSh 6K, hii yote ni vizuri kuambiwa lakini yote ni bure,” aliongeza Kabogo.

“Ahadi za kisiasa wachaneni nazo tafadhali," alisema gavana huyo.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke