Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto asema akichaguliwa 2022 maono yake ya kufufua uchumi yamo katika Bibilia

B784734a8c2410e7 DP Ruto asema akichaguliwa 2022 maono yake ya kufufua uchumi yamo katika Bibilia

Mon, 19 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mfumo wa uchumi unaopendekezwa na William Ruto ni ule unaolenga kuwawezesha wale wanaojishughulisha na biashara ndogondogo, ambazo kwa kawaida hujulikana kwa jina 'hustlers' Ruto alinukuu Zaburi 113: 7-8, kifungu ambacho alidai kinafanana na simulizi zake za hustlerNaibu kiongozi wa chama cha Jubilee alikosoa njia ya kiuchumi ya Rais Uhuru Kenyatta akidai maono yake yananafafanuliwa katika kitabu kitakatifuNaibu wa Rais William Ruto sasa anasema mfomo wa uchumi anaopendekeza wa kuwashughulikia watu wa chini kwenda juu na simulizi zake kuhusu hustler ni mifano hao katika Bibilia.

Mfumo wa uchumi wa Chini Juu ni ule unaolenga kuwawezesha wale wanaojishughulisha na biashara ndogondogo, ambazo kwa kawaida hujulikana kwa jina 'hustlers'.

Akiongea katika Kanisa Katoliki la Saint Patrick huko Kilifi mnamo Jumapili, Julai 18, Naibu Rais alinukuu kifungu katika kitabu kitakatifu, na kusema Hustler nation ni mfano wa maandiko hayo.



Read also

Mimi ni Mke wa Mtu Tafadhali Msipige Simu Baada ya Saa za Kazi, Chifu awaonya Wakaaji

"Tunapotetea mfumo wa uchumi wa Chini Juu, ndivyo biblia inavyosema," alisema Ruto.

Alinukuu Zaburi 113: 7-8, ambayo inaaema: "Humwinua fukara kutoka mavumbini; humnyanyua maskini kutoka unyonge wake, na kumweka pamoja na wakuu,"

Ruto, inavyosema bibilia, wakati wa kampeni zake, alisema serikali ikiwa atafanikiwa kuwa rais, serikali yake itaundwa na watu wa kawaida ambao watakuwa mustari mmoja na matajiri.

Naibu kiongozi huyo wa chama cha Jubilee alikosoa njia ya kiuchumi ya Rais Uhuru Kenyatta akidai maono yake yananafafanuliwa katika kitabu kitakatifu.

Alisema yeyote anayepiga umma wa hustler ni adui ya watu.

Naibu rais alikuwa eneo la Pwani katika hali ya kujipigia debe kuelekea uchaguzi mkuu wa 2022.

Uweledi katika Bible Kwenye taarifa nyingine ya awali, aliyekuwa mbunge wa Starehe, Margaret Wanjiru alimsifu Ruto kwa ufahamu wake mkubwa wa Bibilia.

Akiongea katika kanisa moja la Nairobi Jumapili, Julai 11, Wanjiru alisema Kenya imebarikiwa kuwa na kiongozi kama huyo ambaye hupata kila ahadi yake kutoka katika Biblia.



Read also

Magazeti Jumatatu, Julai 19: Kijiji Chapoteza Watu 13 Katika Mkasa wa Siaya

"Tumebarikiwa kuwa na naibu wa rais ambaye anaweza kunukuu maandiko. Mwenye mapenzi ya Mungu, na Mungu akitusaidia, tutakuwa tukimuapisha kuwa rais wetu ajaye ifikapo mwaka ujao. Kwa hivyo wacha tuendelee katika maombi na kumuunga mkono ambapo tunaweza," Wanjiru alisema huki akishangiliwa na waumini.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke