Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto apuzilia mbali masharti ya IEBC kuhusu wagombea wa uchaguzi

20d9edf8f8f03c1c DP Ruto apuzilia mbali masharti ya IEBC kuhusu wagombea wa uchaguzi

Thu, 17 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Naibu Rais William Ruto amepuzilia mbali masharti ya IEBC ya yanayosema kila anayetaka kuwania kiti serikalini anapaswa kuwa na digriiRuto alisema ataunga mkono marekebisho yanayolenga kufuta kifungu cha 22 cha Sheria ya Uchaguzi kinachowataka wanaojitosa katika siasa kuwa na shahadaIEBC imesisitiza kuwa mahitaji hayo yatazingatiwa katika Uchaguzi Mkuu wa 2022 Naibu Rais William Ruto alishutumu Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kuhusu agizo lake la kuwataka watakaowania nyadhifa za uchaguzi 2022 kuwa na Shahada.

Ruto alisema kuwa agizo la kuwataka wawakilishi wadi (MCA) kuwa na kiwango sawa cha masomo na Wabunge, magavana, na Rais halina msingi wowote.

Akizungumzia Kifungu cha 200 cha Katiba ya Kenya 2010, alisema kuwa jukumu la kutunga sheria kuhusu wasifu wa wagombea nyadhifa na wapiga kura ni la bunge.

Alisema pia kwamba kifungu cha 38 kinaonya dhidi ya kumuwekea mtu masharti ya kumzuia kuwania wadhifa serikalini au kushiriki uchaguzi unapowadia au kura ya maoni.

Ruto alisema kuwa kila wadhifa una sifa zake hususana kuhusiana na masuala ya masomo na iwapo kuna haja ya kusawazisha sifa hizo basi inapaswa kufanywa ndani ya katiba.

Sifa tofauti zinaambatana na majukumu atakayokuwa nayo atakayeshikilia wadhifa huo na vile vile hali ilivyo.

"Haifai kwa asilimia moja tu ya Wakenya kuweza kugombea nafasi za uchaguzi," alielezea DP.

Ruto ameongeza kuwa bunge linatafakari kifungu cha 22 cha Sheria ya Uchaguzi ili kuondoa vizuizi visivyo vya msingi kuwahusu wagombea ambao wanataka kuchaguliwa katika nafasi mbali mbali serikalini.

Aliahidi kuunga mkono kusimamishwa kwa kifungu hicho ili Wakenya wengi waweze kugombea nafasi hizo.

Seneta wa Elgeyo Marakwet Kipchumba Murkomen aliwasilisha msawada kwamba wagombea wanapaswa kutathminiwa iwapo wanajua kusoma na kuandika badala ya kushurtishwa kuwa na digrii.

Murkomen anapendekeza kwamba mtu yeyote anayeweza kusoma na kuandika kwa Kiingereza na Kiswahili, au anayefahamu lugha ya ishara ya anastahili kuruhusiwa kugombania kiuti anachotaka.

Katika muswada uliopendekezwa, Murkomen anasema kuwa mahitaji ya digrii ya chuo kikuu yatafanya uongozi wa kisiasa kuwa hifadhi kwa wasomi na itawanyima haki viongozi kadhaa wenye hekima ambao hawakubarikiwa katika masomo.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke