Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto amtumia Uhuru ujumbe kwenye siku yake ya kuzaliwa

0bcb535e7d1e091f DP Ruto amtumia Uhuru ujumbe kwenye siku yake ya kuzaliwa

Tue, 26 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta, ambaye muhula wake wa pili na wa mwisho unakaribia alitimiza miaka 60 mnamo Jumanne, Oktoba 26 William Ruto alichapisha ujumbe kwenye mitanmdao akimtakia bosi wake heri njema na fanaka anaposhrehekea siku yake ya kuzaliwaWakenya wengi pia walimtumia Uhuru jumbe tamu za kumsherehekea huku wakimshukuru kwa kuweka maslahi ya taifa mbeleNaibu Rais William Ruto amemtakia bosi wake Rais Uhuru Kenyatta heri njema na fanaka anaposherehekea siku yake kuzaliwa kwake.

Kupitia kurasa zake mitandaoni, Ruto aliwataka Wakenya kuungana naye katika kumtakia heri njema kiongozi wa taifa anaposherehekea bathidei yake.

“Tafadhali ungana nami kumtakia kiongozi wetu, rais, mheshimiwa Uhuru Kenyatta, siku njema ya kuzaliwa kwake, na kumwombea mafanikio anapoongoza taifa kuafiki ahadi kubwa zaidi,” alisema.

Niabu rais alimwomba Maulana kumbariki mdosi wake ili aishi miaka mingi duniani na apate kusherehekea bathidei zaidi.

"Mungu akubariki na akuzidishie miaka mingi zaidi duniani ili upare kusherehekea bathidei nyingi hata zaidi," aliongeza.

Wakenya walimiminika mitandaoni na kumsherekea mkuu wa taifa katika siku yake ya kizaliwa.

Nicholas Kosgey alisema;

"Heri njema ya kuzaliwa kwako mheshimiwa. Nimebarikiwa kushiriki siku hii na wewe,"

Cate Kamande alisema;

"Heri njema ya kuzaliwa Uhuru....ni baraka isiyo na kifani kutimia miaka 60 ukiwa na furaha, fanaka na baraka."

Josephine Githaiga;

"Heri njema ya kuzaliwa rais, Mungu akujalie neema unapofungua mwaka mpya na hata zaidi!"

Rose Wangui;

Katika siku hii maalum ya maisha yako, tunakuombea ili Mungu akupe furaha ya milele na nguvu. Tunakutakia maisha marefu Baba. Heri njema ya siku yako ya kuzaliwa. Mola mwenyezi akubariki. Jivinjari kikamilifu,"

Isaac Ouma;

"Heri njema ya kuzaliwa rais wangu mpendwa. Mungu akubariki zaidi na akupe neema ya kuishi miaka mingi ili uwaone wajukuu wako,"

Uhuru alizaliwa Oktoba 26, 1961, kwa baba mwanzilishi wa taifa la Kenya Mzee Jomo Kenyatta na Mama Ngina Kenyatta.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke