Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto amsifia Uhuru, aahidi kuulinda urithi wake

Cef6e1d8d9884d02 DP Ruto amsifia Uhuru, aahidi kuulinda urithi wake

Wed, 20 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

DP alimsifu Uhuru kama kiongozi aliyeleta mabadiliko ambaye sifa na ajenda yake ya maendeleo itampa mwongozo atakapochukua usukani

Uhuru ambaye anapendelea mfumo wa kujenga uchumi kutoka juu kuelekea chini dhidi ya ulw wa DP alionekana pia akipasua kicheko wakati Ruto akimkejeli

Hakikisho la Naibu Rais William Ruto kwa bosi wake, Rais Uhuru Kenyatta, liliwafurahisha waliohudhuria sherehe ya Siku ya Mashujaa kwenye Uwanja wa Wang’uru, Kirinyaga.

Mnamo Jumatano, Oktoba 20, Ruto aliahidi kulinda urithi wa Uhuru baada yake kustaafu mnamo 2022.

DP alimsifu Uhuru kama kiongozi aliyeleta mabadiliko ambaye sifa na ajenda yake ya maendeleo itampa mwongozo kazini.

"Ninawahakikishia kuwa kama naibu wenu kwa miaka tisa, urithi wako, ajenda na mabadiliko ya taifa letu pamoja na mfumo wa kujenga uchumi kutoka chini kuelekea juu utajenga taifa," Ruto alisema wakati umati ulifurahi.

Uhuru ambaye anapendelea mfumo wa kujenga uchumi kutoka juu kuelekea chini dhidi ya DP alionekana pia akipasua kicheko wakati Ruto akimkejeli.

Wakati uo huo, DP alidai kuzungumza kwa niaba ya viongozi wote wa upinzani ambao walikuwa wamehudhuria shetehe hiyo alimhakikishia Uhuru kwamba watashirikiana kazini kwa ajili kuleta amani na maendeleao.

"Ninataka kukuhakikishia kwamba tutalinda urithi wako na kwamba tutaafiki agenda zako zote na miradi ambayo itakuwa bado haijakamilika.

"Tunawasherehekea wale wote ambao walijitolea kumwaga damu kwa ajili ya uhuru wa taifa," alisema huku akiwashukuru wenyeji wa Kirinyaga ambao waliwakaribisha kwa sherehe hizo.

Aidha alimpongeza Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru kwa maandalizi aliyoyafanya ya kuhakikisha sherehe hiyo inafana.

DP alipowasili katika uwanja huo alionekana akimchangamkia kinara wa ODM Raila Odinga.

Wawili hao walisalimina kwa takriban dakika moja baada ya wawili hao kutofautiana hadharani wakati wa kampeni zao nchini katika wiki chache zilizopita.

Kiongozi wa taifa pia alionekana akifurahia huku akipiga gumzi na DP Ruto kabla ya kutoa hotuba yake.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke