Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto amlaumu Rais Uhuru Kenyatta kwa kudororesha uchumi

90c41b83697735b6 Ruto na Kenyatta

Fri, 6 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Naibu Rais William Ruto amedai kwamba Rais Uhuru Kenyatta amedororesha uchumi wa nchiRuto alisema serikali ya Uhuru ilianza kujihusisha na masuala mengine yasio muhimu na kusahau ajenda waliokuwa nayo pamoja na ahadi walitoa kwa WakenyaKulingana na Ruto, viongozi wa NASA wamekuwa wakimpotosha Rais tangu salamu za handishekiAidha, Ruto alikiri awali kwamba alipokonywa majukumu yake na ndio sababu kwa muhula wa pili madarakani hajaweza kufanya kazi kikamilifuNaibu Rais William Ruto amefutilia mbali madai ya Rais Uhuru Kenyatta kwamba amekuwa akifanya kazi usiku na mchana bila ya naibu wake.

Kwa mtazamo wake, Ruto amesema kwamba Rais anawapotosha Wakenya kwani amedororesha zaidi uchumi wa nchi.

Madai haya yanajiri takriban mwezi mmoja baada ya Uhuru kutangaza wazi kwamba kwa muhula wa pili ambao amekuwa madarakani, amefanya kazi bila ya usaidizi wa Ruto.

Kwenye taarifa yake kwa vyombo vya habari Alhamisi, Agosti 5, DP Ruto alisema kwamba serikali ya Uhuru ilianza kujihusisha na masuala mengine yasio muhimu na kusahau ajenda waliokuwa nayo pamoja na ahadi walitoa kwa Wakenya.



Ruto pia alilalamika kwamba alipokonywa majukumu yake na kupeanwa kwa Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga pindi tu baada ya maridhiano kati yao mwaka wa 2018.

"Kwa miaka minne iliyopita tumekuwa tukielezea wasiwasi wetu jinsi Jubilee imetelekeza wajibu wake na kusahau ajenda iliyokuwa nayo lakini hakuna hatua iliyochukuliwa, kwa kifupi ilihujumu ajenda kuu tulizokuwa nazo" Ruto alisema.

Ruto vile vile aliwakashifu viongozi wa muungano wa NASA kwa kumpotosha kiongozi wa taifa hasa kusababisha kucheleweshwa kwa kulipa madeni na kupelekea nchi kufika katika hali iliyomo kwa sasa.

Awali, Ruto alikiri kwamba baada uchaguzi wa 2017 amekuwa akikumbana na changamoto nyingi zingine zilizopelekea yeye kupigwa teke na wandani wa Rais.

Kulingana na Ruto, alifanikiwa kufanya kazi kikamilifu muhula wa kwanza pekee baada yeye kuingia madarani.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke