Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto akanusha kuingiza mahindi nchini kiharamu ili kuwalisha kuku wake

A9215a05cec68afc DP Ruto akanusha kuingiza mahindi nchini kiharamu ili kuwalisha kuku wake

Sat, 17 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Ruto alikanusha madai kwamba alikuwa miongoni mwa watu fulani ambao walidaiwa kuagiza mahindi mnamo 2010

- Naibu kiongozi huyo wa Jubilee alishikilia kwamba anawalisha kuku wake nafaka ambayo anaikuza katika shamba lake la Sugoi

- Mnamo Februari 2010, wakati kiongozi wa ODM Raila Odinga alikuwa waziri mkuu, alimsimamisha kazi Ruto na aliyekuwa waziri wa Elimu wakati huo Sam Ongeri

Naibu Rais William Ruto amekana vikali kuwahi husika katika biashara ya uingizaji mahindi nchini wakati alikuwa waziri wa Kilimo.

Ruto alikanusha madai kwamba alikuwa miongoni mwa watu fulani ambao walidaiwa kuagiza mahindi mnamo 2010, na hivyo kutumbukiza wakulima wa mahindi katika matatizo.

Akiongea na Citizen TV, naibu kiongozi wa Chama cha Jubilee alisisitiza anatumia tu nafaka kama chakula cha kuku kwenye shamba la kuku katika shamba lake la Sugoi, kaunti ya Uasin Gishu.

“Sijawahi kuagiza hata nafaka ya mahindi kutoka nje. Ninalima mahindi yangu mwenyewe ambayo nawalisha kuku wangu. Niliacha kuuza mahindi kwa NCPB muda mrefu uliopita, ” alisema.

Mnamo Februari 2010, wakati kiongozi wa ODM Raila Odinga alikuwa waziri mkuu, alimsimamisha kazi Ruto na aliyekuwa waziri wa Elimu wakati huo Sam Ongeri kuhusu kashfa ya mahindi.

"Ninachukua hatua hii kwa sababu ya uchunguzi ambao umewamulika wawili hao. Wanapaswa kudadisiwa kwa kina," Raila alisema katika taarifa.

Baadaye jioni hiyo, Ruto alisema haendi popote kwani alifahamu fika mamlaka iliyomuajiri iliyosimamiwa na Mwai Kibaki.

“Nimesoma kwa uangalifu sana barua yangu ya uteuzi ... na mamlaka ya uteuzi iko wazi kabisa. Sijapokea mawasiliano yoyote kutoka kwa mamlaka ya kuteua kama waziri wa Kilimo na kwa hivyo nitaendelea kutekeleza majukumu yangu, " alijibu.

Mnamo mwaka wa 2018, Mbunge wa Nandi Hills Alfred Keter na mwenzake wa Chereng'ani Joshua Kutuny walidai Ruto ndiye chanzo cha shida ambazo wakulima wa mahindi walikuwa wakikabiliana nazo.

Wawili hao walidai Ruto alikuwa akiwashauri wakulima kuacha kilimo cha mahindi na kuanza kulima parachichi na mazao mengine kwa sababu alitaka asalie kwenye soko la mahindi peke yake.

Akiongea kwenye mkutano wa wakulima huko Eldoret, Keter alidai DP alikuwa akipanga kulima zaidi ya ekari 500,000 za mahindi nchini Congo kwa nia ya kuagiza mazao hayo Kenya.

"Wewe (Ruto) sasa umehamia Congo ambapo unapanga kulima zaidi ya ekari 500,000 za mahindi ... halafu unatuambia kuhusu parachichi? Hata hiyo parachichi, tunajua una kiwanda pia huko Botswana ambapo unasindika, " Keter alisema.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke