Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto afichua kikao tete kati yake, Rais Uhuru na mkuu wa ujasusi

Ba2963b6a6d2aea4 DP Ruto afichua kikao tete kati yake, Rais Uhuru na mkuu wa ujasusi

Sat, 17 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- DP Ruto alisema kwenye kikao hicho alitaka mkurugenzi wa ujasusi nchini kutoa ushahidi kuwa amekuwa 'akijifanya rais'

- Alisema kama wajibu wake tangu 2013 amekuwa akitekeleza kazi ya naibu rais bila kupita mipaka

- Wandani wa Rais Kenyatta wamekuwa wakisema DP huendesha serikali mbadala kupitia afisi yake mtaani Karen

Naibu Rais William Ruto Alhamisi Aprili 15 alifichua mengi wakati wa mahojiano yake na runinga ya Citizen.

Akiongea na mtangazaji Linus Kaikai, DP alifungua roho kuhusu masaibu yake ndani ya serikali ambayo alisaidia kuiunda.

Ruto alisema amekuwa akisingiziwa kumhujumu Rais Uhuru Kenyatta serikalini kiwango cha maafisa wakuu kuibua maswali.

DP alisema ni hali ambayo ilifanya yeye kuitwa na Rais kuhusu suala hilo ambapo lilichambuliwa kwa undani.

"Tulifanya kikao na Rais na kumuuliza iwapo nimewahi kumhujumu kwa namna yoyote, na akaniambia hakuna kitu kama hicho," alisema Ruto.

DP alisema walikuwa katika kikao hicho tete na Rais pamoja na mkurugenzi wa ujasusi nchini na kutaka ushahidi wowote wa kuwa alijifanya kama rais.

"Niliambia mkurugenzi wa ujasusi nchini atoe ushahidi wowote kuwa mimi nimewahi kumhujumu au kujifanya rais aidha kwenye umma au hata kwingineko. Nilitaka watoe," alisema Ruto.

Wandani wa Rais Uhuru wamekuwa wakimlima DP na kusema amekuwa akifikiria yeye pia ni rais.

Aidha wamekuwa wakimkosoa DP kwa madai ya 'kuendesha serikali mbadala' na ile ya Rais na hivyo kuleta msukosuko wa uongozi.

Hata hivyo, alikanusha hayo na kusema amekuwa mwaminifu kwa Rais wakati wote licha ya magumu aliyoonjeshwa.

"MImi nimekuwa mwaminifu na mwenye heshima kwa Rais wakati wote," alisema DP wakati wa mahojiano hayo ya Kakai Alhamisi Aprili 15.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke