Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto adokeza ni lini pamoja na wandani wake wataondoka Jubilee

15e93e942ecc75fd DP Ruto adokeza ni lini pamoja na wandani wake wataondoka Jubilee

Fri, 6 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Naibu Rais William Ruto amesema wanasiasa wa Huster Nation wamepata makao mapya na wataondoka Jubilee wakati ufaao Ruto alidai chama cha Jubilee kimesabaratika na haoni matumaini iwapo kitaunganika tenaAidha, Ruto amesema hatajiuzulu kama naibu Rais jinsi anavyoshinikizwa na baadhi ya wapinzani wakeNaibu Rais William Ruto amethibitisha kwamba yeye pamoja na wandani wake wa mrengo wa Tanga Tanga wako tayari kuondoka kwenye chama tawala cha Jubilee.

Akizungumza akiwa kwenye hafla ya siasa nyumbani kwake mtaani Karen Alhamisi, Agosti 5, Ruto alitangaza wazi kwamba nyumba ya Jubilee imebomoka sana kiwango ambacho haiwezi ikafanyiwa ukarabati.

Ruto alisema wanasiasa wa Huster Nation wamepata makao mapya na wataondoka Jubilee wakati ufaao na ni hivi karibuni.

"Watu hufanya uamuzi wakati ufaao na wanapofikiria uamuzi tofauti unahitajika, kwa sasa sisi sio wageni mahali popote, tunajiunga na vyama tukitaka na tunaondoka tukitaka, hakuna mtu anapaswa kutuuliza kwani nini hatujaondoka," Ruto alisema.

Ruto alisema haya baada ya kuuliza kinamchozuia kuondoka kwenye chama ambacho serikali yake inaamini hajatekeleza majukumu yake kama Naibu Rais.

Read also

Moto Gikomba: Wafanyabiashara Katika Soko la Gikomba Wapata Hasara

Ingawa Ruto hakutaka ni lini atajiuzulu, lakini kulingana na fununu kutoka kwa wandani wake wa karibuni waliomo ndani ya chama cha UDA, inasemekana huenda ikawa mwishoni mwa mwaka huu.

Baadhi ya viongozi akiwemo kiongozi wa chama cha Narc Kenya Martha Karua wamekuwa wakimshinikiza Ruto kujiuzulu iwapo hawezi akaridhiana na bosi wake ambaye ni Rais Uhuru Kenyatta.

" Huu ni mfano mbaya sana, wote wawili wanawezajiuzulu na uchaguzi mdogo ufanywe, walichaguliwa kama kitu kimoja na wanapaswa kufanya kazi pamoja," Karua alisema.

Vigogo wengine ambao wamekuwa mstari wa mbele kumtaka Ruto ajiuzulu ni kiongozi wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka na Gavana wa Machakos Alfred Mutua.

Hata hivyo, licha ya kupigwa vita hivi vyote, Ruto alisema mwezi Aprili 2021, kwamba hatajiuzulu hata uhusiano wake na Rais ukizidi kudhoofika.

" Mimi nilichaguliwa na sitakubali kuwapa fursa mahasidi wangu kusherehea nikijiuzulu. Siwezi jiuzulu," Ruto alisema Alhamisi, Aprili 15.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Read also

Magazeti Ijumaa Julai 6: DP Ruto Asema Atachomoka Kutoka Serikali Wakati Ukifika

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke