Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto adai Uhuru anapoteza muda kujali NASA badala ya kuwajali Wakenya

666cb01200710680 DP Ruto adai Uhuru anapoteza muda kujali NASA badala ya kuwajali Wakenya

Tue, 13 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

William Ruto aliwashutumu wakuu wa NASA kwa kumtumia Rais Uhuru kuanza kazi zao za kisiasaRuto alisema wakuu wa NASA hawakubaliani kwa sababu ni wabinafsi na wenye tamaaAlibainisha kuwa rais alipaswa kuhudumia masilahi ya Kenya na sio yale ya wakuu wa NASARais Uhuru, wakati wa ziara yake Ukambani, alidokeza juu ya kuungana tena kwa muungano wa NASA kabla ya 2022Naibu Rais William Ruto sasa anataka viongozi katika National Super Alliance (NASA) kusuluhisha tofauti zao bila kumshirikisha Rais Uhuru Kenyatta.

Rais kuwatumikia WakenyaRuto, ambaye alizungumza huko Kiambu Jumapili, Julai 11, alisema Rais Uhuru Kenyatta hakuchaguliwa katika ofisi hiyo kuwatumikia wakuu wa muungano wa NASA bali Wakenya.

Alidai nchi imeshindwa kujiendeleza kiuchumi kwa sababu rais amegeuka kuwa msuluhishi katika mapambano yanayoendelea katika NASA.

“Je, tulimchagua rais kwenda kuunganisha muungano wa NASA? Wanamsumbua rais ambaye badala ya kuwahudumia Wakenya sasa analazimika kushughulikia masuala yanayohusu watu watano ambao ni wachoyo, wa kujivuna na wasio na adili kwa kiwango ambacho Kenya haiwezi kwenda mbele," DP alisema.



Read also

Tharaka Nithi: Watu Watatu Wafariki Dunia Baada ya Kunywa Pombe ya Asali

Magazeti Jumanne, Julai 13: Maseneta Wataka Chanjo ya COVID-19 kuwa Lazima kwa Wakenya

Tamaa ya madarakaAlizidi kuwashutumu wakuu wa NASA, ambao ni kiongozi wa ODM Raila Odinga, Kalonzo Musyoka wa Wiper, Musalia Mudavadi wa ANC na Moses Wetangula wa Ford Kenya, kwa tamaa yao ya kutaka madaraka.

“Rais sasa ameingia katika msukumo na kuvuta na wakuu hawa wa Nasa ambao wametofautiana juu ya nani wa mbele. Kila mtu amejaa pupa; huyu anataka nguvu, mwingine anasema hawezi kufanya kazi na huyu, na mwingine anasema nina idadi hizi za risasi,” aliongeza kusema.

Ujumbe wake ulijiri siku mbili baada ya Rais Uhuru kuzuru eneo la Ukambani akiwa na Raila na Kalonzo, ambapo alidokeza kuwaleta pamoja viongozi hao kabla ya 2022.

Ni wakati wa ziara yake ya Ukambani ambapo mazungumzo ya kufufua NASA muungano unaoonekana kufa yalipoibuka, na Raila akimtaka Rais Uhuru pia ajiunge na muungano huo wakati mazungumzo ya kuufufua yanapoanza.



Read also

Ruto Amjibu Rais Baada ya Kumkashifu kwa Kuwachochea Wakenya

Hatua ambayo imeonekana kumkasirisha naibu rais kwa kuwa hali hiyo huenda ikamnyima nafsi ya wazi kuingia Ikulu.

Lakini hata wakati Raila anafufua mazungumzo ya kuwakutanisha NASA, Kalonzo na Mudavadi wanashikilia msimamo wao wa kutaka kuwa wagombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke