Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto achemka baada ya rafikiye Harun Ayadin kukamatwa

16a93054d35904bf DP Ruto achemka baada ya rafikiye Harun Ayadin kukamatwa

Sun, 8 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Ruto Jumamosi aliwaka moto akisema serikali inawlaenga marafiki wake na kila aina za hujumaAliwataka wapinzani wake serikali kumkabili yeye akisema kinachoendelea kwa sasa ni marafiki wake kuhangaishwa bureRuto aliwaka moto baada ya mfanyabiashara kutoka Uturuki Aydin kukamatwa akihusishwa na vitendo vya ugaidiNaibu Rais William Ruto Jumamosi Agosti 7 alikashifu serikali kwa kumkamata mfanyabishara Harun Aydin ambaye ni rais kutoka Uturuki.

Ruto alisema Kenya itaharibu sifa yake kwa kuwahusisha wawekezaji na uhalifu wa kigaidia kama vile imemfanyikia Aydin.

Akiongea Karen, Ruto alisema kinachoendelea ni vita vya kisiasa dhidi ya marafiki wake akisema hilo halifai.

Aliwataka mahasimu wake katika siasa kumkabili yeye badala ya kuhangaisha watu wanaotengamana na yeye.

"Sasa hawa watu wanataka kutuambia kama huna God father, kama wewe hujulikani, kama wewe si mtoto wa mtu fulani huwezi kufanya biashara Kenya hii.



"Ukifanya ya boidaboda wanasema wewe ni mhalifu, ukifanya ingine kule Nyamakima wanasema wewe ni contraband. Ukifanya kama ile ya Keroche, unatumiwa KRA," alisema Ruto.



Read also

DP Ruto Amkashifu Rais Uhuru Kenyatta kwa Kudororesha Uchumi wa Nchi

DP alihoji ni vipi raia ambaye anatabulika na serikali yake Uturuki ametajwa kuwa mshukiwa wa kigaidi.

"Saa hii hata wawekezaji ambao wako na kibali na wanajulikana na serikali zao tunasema ni magaidi kwa sababu tuko na nia duni za kisiasa. Hii ni kusambaratisha taifa letu la Kenya na mnaturudisha nyuma kwa umaskini mkitafuta nia zenu za kibinafasi," alisema DP.

Aydin amekuwa akigonga vichwa vya habari tangu Julai 3 wakati safari ya DP kuenda Uganda ilitibuka alipofika uwanja wa ndege wa Wilson.

Ripoti ziliibuka kuwa afasi hiyo ilitibuka kwa sababu Aydin alikuwa mmoja wa wasafiri katika orodha ya waliokuwa wakiandamana na DP.

Maafisa wa kupambana na Ugaidi walimkamata Jumamosi Agosti 7 alipoingia nchini kutoka Uganda na akazuiliwa kwa mahojiano.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke