Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto aahidi kuendeleza atakapoishia Rais Kenyatta

8f1593865e196402 DP Ruto aahidi kuendeleza atakapoishia Rais Kenyatta

Thu, 4 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Naibu Rais William Ruto ameahidi kuendelea na Ajenda Nne Kuu za Rais Uhuru Kenyatta iwapo atachaguliwa Ruto alikariri msimamo wake kwamba ajenda nne kuu zilizimwa wakati wa salamu za maridhiano baina ya Uhuru na kinara wa ODM Raila Odinga.

Ruto pia aliwacheka wale wanaotishia kumwondoa kutoka wadhifa wa naibu kiongozi wa chama cha Jubilee Naibu Rais William Ruto ameapa kuendelea na ajenda ya maendeleo ya Rais Uhuru Kenyatta iwapo atachaguliwa kuwa rais mwaka wa 2022.

Akiongea wakati wa ziara eneo la Mlima Kenya, Ruto aliahidi kuendeleza ajenda nne kuu anazodai zilizimwa wakati wa salamu za maridhino baina ya Uhuru na kiongozi wa Orange Democratic Movement (ODM) Raila Odinga.

"Mwaka ujao, ahadi zote ambazo bado hatujatimizia katika ajenda kuu nne tumepanga na kujumuisha katika mfumo wa kutoka chini kwenda juu ili tuendelee kusonga mbele kama tulivyokubaliana hapo awali," Ruto alisema.

Agenda hizo ni Nne Kuu Afya kwa Wote, Makazi Bora, Ukuaji wa Viwanda na Utoshelezo wa Chakula.

Ruto alizidi kuwacheka wale wanaotishia kumwondoa katika wadhifa wa naibu kiongozi wa chama cha Jubilee, akisema hakuna tija kwani chama hicho kilikoma kuwepo na kupigwa mnada kwa upinzani.

"Baadhi ya watu bado wanakutana ili kutujadili. Ni nini haswa mnasema? Chama chenyewe kilipoteza umaarufu kitambo sasa mnatuambia nini? Nadhani kitaingia kwenye kumbukumbu za Kitabu cha Guinness kwamba hapo zamani kulikuwepo na chama, chama tawala ambacho kilichoporomoka, kikafa na hatimaye kuuzwa kwa upinzani. Hiyo ni historia ya aina gani?" Ruto alisema.

Aidha waliwasuta wakoasoaji wake na kusema kwamba walisambaratisha chama baada ya kumkaribisha mtu wa vitendawili na sasa wanang'ang'a kufufua kilichoangamia tayari.

Chama tawala cha Jubilee kinapanga kuandaa Kongamano la Wajumbe wa Kitaifa (NDC) ambalo linasubiriwa kwa hamu.

Katibu mkuu wa chama hicho Raphael Tuju alitangaza Jumatatu, Novemba 1, baada ya kukutana na Kamati ya Kitaifa ya Usimamizi (NMC).

Kongamano hilo linaonekana kuidhinisha mkataba na aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga na kuanzisha kuondolewa kwa Ruto kama naibu kiongozi wa chama.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke