Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto Akishambulia Chama cha Ford Kenya, Asema ni Kinanguruma tu Kijijini

Eb878f2906696c1e DP Ruto Akishambulia Chama cha Ford Kenya, Asema ni Kinanguruma tu Kijijini

Thu, 25 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Ruto alisema chama cha FORD Kenya hakiwezi kupata ushindi wowote nje ya eneo bunge la Kabuchai

- Pia alivichana vipande vyama vya ANC na Wiper, akisema ni vya kikabila

- Naibu rais alisema chama chake cha UDA kina sura ya kitaifa na kwamba kinapania kuwaungamisha watu wa tabaka mbali mbali kote nchini

Naibu Rais William Ruto amekishambulia chama cha FORD Kenya ambacho wiki chache kiliingilia chama chake cha United Democratic Movement (UDA) katika uchaguzi mdogo wa Kabuchai.

Ruto alidai chama cha Simba ambacho kinaongozwa na seneta wa Bungoma Moses Wetang'ula, na abacho kimehudumu kwa muda mrefu nchini, kilikuwa kikinguruma tu kijijini.

Ruto, ambaye alikuwa akizungumza kwenye Jalongoo TV Alhamisi, Machi 25, alisema FORD Kenya haiwezi kushinda kiti chochote cha kitaifa isipokuwa kauntiya Bungoma tu.

"Mahali pekee ambapo FORD Kenya inaweza kupata ushindi ni Kabuchai tu kwa sababu ni chama cha kijiji ... kiongozi wa chama anatoka Bungoma, katibu mkuu anatoka sehemu iyo hiyo na ndio sababu hawawezi kumsimamisha mgombea huko Machakos.

"Hata katika kaunti hiyo ya Bungoma, Jubilee ina viti vitatu na FORD Kenya ina viti vitatu pia. Lakini kumbuka hawana kiti kingine chochote mahali pengine popote, " Ruto alisema.

Naibu Rais pia alivishusha hadhi chama cha Amani National Congress (ANC) kinachoongozwa na Musalia Mudavadi na Wiper Democratic Movement chake na Kalonzo Musyoka.

Kulingana na DP, vyama hivyo wiwili vilikuwa vya kikabila vinavyotumiwa na "machifu wa kabila" kutafuta nguvu.

"Hivi ni vyama vya kikabila. Wiper anaweza kushinda viti vichache tu Ukambani wakati ANC inaweza kushinda viti kadhaa huko Kakamega," alidai DP.

Alitetea chama chake kipya cha UDA akisema ni mavazi ya kitaifa na mipango ya kuleta kila mtu bila kujali kabila lake, mkoa au asili.

Alikitetea chama chake kipya cha UDA akisema kina sura ya kitaifa na mipango ya kuwaunganisha watu wa tabaka mbali mbali bila kujali kabila, mkoa au asili.

Ruto alitetea chama hicho ambacho wengi walikidhalilisha kutokana na matokeo yake ya uchaguzi mdogo uliofanyika majuzi katika sehemu mbali mbali nchini.

"Tofauti kati yetu na washindani wetu ni sisi ni vuguvugu la kitaifa. Vuguvugu la kitaifa haimainiihsi unamuweka mgombea uwanjani kwa sababu una nafasi ya kushinda tu.

"Mnaweza kujiuliza kwa nini Wiper na ANC hawakuwa na wagombea huko Kabuchai Sisi sote tunataka kuwa na sura ya kitaifa, tunataka kujenga chama cha kitaifa na hiyo inamaanisha tunaweka wagombea wa kuimarisha msingi yetu kule mashinani sio kushinda tu," alisema DP.

Mudavadi, Kalonzo, Wetang'ula, na Gideon wanafanya kazi pamoja chini ya muungano wa One Kenya Alliance.

Ripoti zinaonyesha kuwa wanaungwa mkono na Rais Uhuru Kenyatta, ambaye pia anasemekana anafanya mazungumzo na viongozi wa pwani kujiunga nao.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke