Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Crisis Meeting: Jubilee kukutana Jumatano kujadili kichapo cha Kiambaa

2b34205e959f3781 Crisis Meeting: Jubilee kukutana Jumatano kujadili kichapo cha Kiambaa

Sun, 18 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wandani wa Rais wanasema wameingiwa na kibaridi cha kisiasa baada ya Jubilee kubwagwa KiambaaKikao cha dharura kimeitishwa ambapo wanachama watakutana Jumatano Julai 21 ParklandsUchaguzi mdogo wa Kiambaa na Juja ndio umewapa kibaridi wandani wa Rais wakihofia huenda wafuasi wa Mt Kenya watawahepa kisiasaChama cha Jubilee kimeitisha kikao cha dharura Jumatano Julai 21 katika makao yake makuu mtaani Parklands.

Wanajubilee watakutana ili kujadili matokeo ya chama hicho katika chaguzi ndogo zilizopita na sababu zake kushindwa.

Duru zimearifu baadhi ya wanachama wa Jubilee ambao ni wandani wa Rais Uhuru Kenyatta wanataka ahudhurie kikao hicho.

Kikao hicho kimetajwa kuwa muhimu kwa maisha ya chama cha Jubilee ambacho kiko serikalini lakini kinashindwa na chama kinda kama UDA kwenye uchaguzi mdogo.



Baadhi ya wandani wa Rais wanasema wako na wasiwasi kuhusu kubadilika kwa siasa za Mlima wakitaka hatua za dharura kuchukuliwa.



Read also

NIS Ilionya Rais Uhuru Kwamba Jubilee Itabwagwa na UDA Kiambaa

Duru zimearifu wanataka Rais pia ajitokeze na kuwahakikishia kuwa yuko na mpango kabambe wa siasa za 2022 wasije wakabaki peke yao na kuzama.

Uchaguzi mdogo wa Kiambaa na Juja ndio umewapa kibaridi wandani wa Rais wakihofia huenda wafuasi wa Mt Kenya watawahepa kisiasa.



Gavana wa Kirinyaga, Anne Waiguru amesema mabadiliko katika usimamizi wa chama cha Jubilee ndio dawa pekee ya aibu waliopata kwa kubwagwa katika chaguzi ndogo kadhaa.

“Wafuasi halisi wa Jubilee hawana furaha na hatua za dharura zinafaa kuchukuliwa kuzuia kisiporomoke,” Waiguru aliambia gazeti la Taifa Jumapili Julai 18.

Tayari wabunge kama Kanini Kega na Ngunjiri Wambugu wamejitokeza na kusema katibu wa Jubilee Raphael Tuju na David Murathe wanafaa kuondoka kwenye uongozi wa chama.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.



Read also

Murathe na Tuju Pabaya Baada ya Jubilee Kufinywa na UDA Kiambaa

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke