Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeripoti kumalizika kwa mlipuko wa Ebola mara baada ya kutokuwepo kwa wangonjwa wapya kwa muda siku 42.
Mlipuko huo wa ghafla ulinza mwezi Oktoba 08, 2021 mara baada ya kuripotiwa kwa kifo cha mtoto menye umri wa miaka mitatu katika jimbo la Kivu Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.
Tukio hili lilifuwatiwa na kesi nane mpya za wagonjwa wa Ebola sambamba na vifo tisa katika neneo hilo la Kivu mfululizo ndani ya miezi miwili huku waathirika wakubwa wakiwa ni watoto walio na umri chini ya miaka mitano.
Nalo Shirika la Afya Duniani, WHO limethibitisha kutokuwepo kwa maambukizi mengine mapya ndani ya siku hizo tajwa 42 tangu ugonjwa huo ugundulike.