Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Congo Brazzaville yakanusha madai ya jaribio la mapinduzi, yaomba utulivu

Congo Brazzaville Yakanusha Madai Ya Jaribio La Mapinduzi, Yaomba Utulivu Congo Brazzaville yakanusha madai ya jaribio la mapinduzi, yaomba utulivu

Mon, 18 Sep 2023 Chanzo: Bbc

Serikali ya Congo-Brazzaville imekanusha ripoti za jaribio la mapinduzi dhidi ya Rais Denis Nguesso, ambaye amekuwa madarakani kwa miaka 39.

Inafuatia ripoti za mitandao ya kijamii ambazo hazijathibitishwa kuwa jeshi lilikuwa likijaribu kumuondoa madarakani kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 79 ambaye kwa sasa yuko New York kwa kikao cha 78 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

"Serikali inakanusha taarifa hizi za uwongo," Waziri wa Habari Thierry Moungalla alichapisha kwenye X (zamani Twitter) siku ya Jumapili.

"Tunahakikishia umma kuwa hali ni tulivu na tunawaomba watu kufanya shughuli zao kwa utulivu."

Tovuti ya serikali pia ilichapisha taarifa ya kukanusha ripoti za jaribio la mapinduzi.

Kumekuwa na wimbi la mapinduzi barani Afrika katika miezi ya hivi karibuni, huku ya hivi punde zaidi katika nchi jirani ya Gabon, ambako jeshi lilinyakua mamlaka mwezi Januari.

Bw Nguesso aliingia madarakani katika nchi hiyo ya Afrika ya kati inayozalisha mafuta katika mapinduzi ya kijeshi mwaka wa 1979. Alipoteza uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi nchini Kongo mwaka 1992 lakini akapata tena mamlaka mwaka 1997 baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Kiongozi huyo wa Kongo ndiye rais wa tatu kwa muda mrefu zaidi barani Afrika, baada ya Teodoro Obiang wa Equatoguine na Paul Biya wa Cameroon.

Chanzo: Bbc