Mon, 12 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Mawasialiano ya Rais Mteule imezuia vyombo vya habari vya nchini humo kurusha hafla ya kuapishwa kwa William Ruto na kutoa haki za kipekee za utangazaji kwa Multichoice Kenya Ltd.
Tangazo hilo limepokelewa kwa hisia tofauti na wanahabari wa ndani na mashirika ya habari, huku gazeti la Daily Nation likimshutumu Ruto kwa kupoteza fursa ya kuonesha utawala bora.
Timu ya Mawasiliano ya Rais Mteule imeshutumu vyombo vya habari vya nchini humo kwa kuegemea upande wa Raila na Rais Uhuru na kususia mikutano ya Muungano wa Kenya Kwanza wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live