Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Chameleone ashindwa Umeya

388d0d1782dae3fb5995e9d3c34c27a6 Chameleone ashindwa Umeya

Mon, 25 Jan 2021 Chanzo: habarileo.co.tz

MEYA Elias Lukwago wa Chama cha FD ameweza kutetea kiti chake cha Umeya wa jiji la Kampala kwa kuwapiku wapinzani wake 10, akiwemo msanii Joseph Mayanja ‘Jose Chameleone’.

Msimamizi wa uchaguzi Ruwaga kitongoji cha jiji la Kampala ndiye aliyekuwa mhusika mkuu katika kuhesabu kura kwenye matokeo ya uchaguzi wa Meya wa jiji la Kampala.

”Ndugu zangu sina cha kuwaambia nina furaha kubwa watu wangu, hapa nyumbani na wakazi wote wa jiji la Kampala asanteni sana”.

Lukwago alishinda karibu kata zote tano za wilaya ya Kampala kwa mujibu wa matokeo ya mwanzo yaliotolewa katika kata zote.

Wakati huo huo, Mahakama Kuu Kampala inatarajiwa kusikiliza ombi la Robert Kyagulanyi kuachiwa huru na vikosi vya ulinzi vinavyomzuia nyumbani kwake.

Chanzo: habarileo.co.tz