Chama cha UDPS cha Rais wa Congo, Felix Tshisekedi, kimefanikiwa kuchukua viti 66 kati ya 500, vya Bunge la nchi hiyo, katika Uchaguzi uliofanyika Desemba 2023, ikiwa ni sawa na 12% ya viti vyote kwenye Bunge la nchi hiyo.
Chama cha UDPS cha Rais wa Congo, Felix Tshisekedi, kimefanikiwa kuchukua viti 66 kati ya 500, vya Bunge la nchi hiyo, katika Uchaguzi uliofanyika Desemba 2023, ikiwa ni sawa na 12% ya viti vyote kwenye Bunge la nchi hiyo. Idadi hiyo inakifanya Chama cha UDPS, kuwa na viti vingi zaidi kwenye Bunge hilo, huku vyama vinavyoongozwa na baadhi ya washirika wa Tshisekedi akiwemo Spika wa Seneti Modeste Bahati Lukwebo, Waziri wa Ulinzi Jean Pierre Bemba na Waziri wa Uchumi Vital Kamerhe vikifanikiwa kushinda zaidi ya viti 80.