Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Chama cha Ford Kenya Chavunja Uhusiano na NASA

23044983736d7d6a Chama cha Ford Kenya Chavunja Uhusiano na NASA

Sun, 1 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Chama hicho kinachoongozwa na seneta wa Bungoma Moses Wetang'ula ndicho cha hivi karibuni kuondoka katika muungano wa NASA Vyama vingine ambavyo vimejiondoa katika muungano huo ni Amani National Congress (ANC), Wiper Democratic Movement na Orange Democratic Movement (ODM) Kamati Kuu ya Kitaifa ya Ford Kenya (NEC) ilifanya mkutano katika makao makuu ya chama hicho Nairobi Jumamosi, Julai 31 Chama cha Ford Kenya kimefanya uamuzi wa kuondoka katika muungano wa National Super Alliance (NASA).

Chama hicho kinachoongozwa na Moses Wetang'ula ni cha hivi karibuni kuvunja uhusiano wake na NASA kuondoka baada ya Amani National Congress (ANC), Wiper Democratic Movement na Orange Democratic Movement (ODM) kuondoka.

Wetang'ula alitangaza kuchukua hatua hiyo baada ya kufanya mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na wanachama waliokubaliana kwa kauli moja kuvunja uhusuiano na NASA.

Akihutubia wanahabari akiwa Simba House kaunti ya Nairobi Jumamosi, Julai 31, Wetang'ula alihimiza Raila na ODM kufanya vivyo hivyo.



Read also

Aliyekuwa Naibu Gavana Jonathan Mueke Apanda Wheelbarrow, Ajiunga na Hustler ya DP Ruto

''Umoja wa watu wa Kenya ni jambo kuu katika harakati zetu za uongozi. Katika hali hiyo hatutaki kumfungia mtu yeyote nje. Tuliunda muungao wa NASA kwa sababu tulikuwa na maazimio yaliyooana na ndio maana sasa tumegura na kuelekea One Kenya Alliance (OKA)kwa sababu ya umoja wa maendeleo, tunaalika ODM na uongozi wake," Wetang'ula alisema.

Seneta huyo alisema iwapo ODM itafanya maamuzi ya kujiunga na OKA basi inapaswa kuweka majivuno kando.

'Tunahitaji kuendelea pamoja. Na ikumbukwe kwamba siasa kuhusu jinsi mtu anavofaidika. Siasa haipaswi kuongozwa na uadui wala kinyongo. Wapinzani wa jana ni washirika wa leo. Wapinzani wa kisiasa wa jana ni washirika wa kisiasa," Wetang'ula aliongeza.

Mnamo Alhamisi, Julai 29 baraza la ODM lilisema limefanya uamuzi wa kugura muungano wa NASA kujipanga kutafuta narafiki wapya wa siasa.

"Bado tunashikilia kwamba NASA imepitwa na wakati. Ili kudhihirisha zaidi ukweli huu, Kamati ya Utendaji ya Kitaifa (NEC) ya ODM leo imeamua kuhama NASA," ilisema taarifa iliyosomwa na katibu mkuu wa chama hicho Edwin Sifuna.

Read also

Raila Amefanya Uamuzi wa Busara Kutema NASA - Moses Kuria Asema

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke