Wed, 1 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Chakula cha msaada kilichopelekwa katika Jimbo la Kirinyaga nchini Kenya linalokabiliwa na njaa kali, kimeibwa na kusababisha wakazi wa eneo hilo kukesha kwenye ofisi za serikali.
Vurugu kubwa zinadaiwa kuibuka majira ya usiku, baada ya watu kusubiri sana chakula lakini mwisho wakaishia kuambiwa kwamba magunia kumi yalikuwa hayafahamiki yalipo.
Mbunge wa Kirinyaga, Gachoki Gitari akaingilia kati na kuwatuliza wananchi, akiahidi kushughulika na wote waliosababisha chakula hicho kiibiwe.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live