Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Caroline Kangogo azikwa kama raia, familia yatii ombi la kuvishwa kama Bi Harusi

Aa23cf5078428dcd Caroline Kangogo azikwa kama raia, familia yatii ombi la kuvishwa kama Bi Harusi

Fri, 30 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Hakukuwa na kikosi cha maafisa wenzake kumpa mkono wa buriani kama ilivyo kawaida ya afisa anayefariki kaziniFamilia yake ilitii ombi lake la kuzikwa akiwa amevalia vazi linalovalishwa bi harusi siku ya kufunga pingu za maishaKangogo alipatikana akiwa amejipiga risasi katika bafu la nyumbani kwao Julai 16 asubuhi baada ya kuwa mafichoni kwa siku tanoAfisa aliyejimaliza Caroline Kangogo amezikwa nyumbani kwao katika kijiji cha Nyawa kaunti ya Elgeyo Marakwet.

Kangogo alizikwa kiraia kwani wenzake katika idara ya polisi hawakufika kumpa mkono wa buriani kupitia guaride la heshima.

Kwa kawaida, afisa wa polisi huzikwa na wenzake ambapo wao hubeba jeneza pamoja na kufunikiwa kwa bendera ya kikosi chake.

Hata hivyo, mazishi ya afisa huyo wa kike yalikuwa ya kiraia kwani hata mwili ulitolewa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwa gari la kubeba maiti bila kuongozwa na gari la polisi.

Milio ya risasi haikuwepo pia kama vile huwa kawaida ya mazishi ya maafisa wengine wa polisi ambapo risasi 21 hufyatuliwa.



Read also

Picha Tamu za Christine Ambani Aliyeuawa Ndani ya Lojing'i Githurai

Wakazi walipata nafasi ya kuutazama mwili wa Kangogo ambapo alikuwa amevalishwa nguo ya harusi kama alivyoagiza wazazi wake.



Kupitia jumbe alizoacha, afisa huyo alisema avalishwe nguo nyeupe ya harusi akitaja mazishi yake kama siku kubwa kwake.

Alipatikna akiwa amefariki Julai 16 baada ya kusakwa kwa muda akihusishwa na mauaji ya watu wawili.

Familia yake hata hivyo ilimkumbuka kama afisa aliyekuwa mpole na mwenye bidii wakisema ni 'Mkono wa Bwana ambao' umemuondoa duniani.

Afisa huyo alizaliwa mwaka wa 1987 kabla ya kujiunga na kikosi cha polisi 2008 na kupanda vyeo huku akijulikana kama stadi wa kupiga risasi.

Julai 12 aligeuka mshukiwa baada ya kudai kummaliza afisa mwenzake John Ongweno katika kituo cha polisi cha Kasarani Nakuru.

Je, unayo taarifa ya kusisimua mbayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke