DCI na idara zingine za usalama zinamchunguza Caroline Kangogo ambaye anatuhumiwa kuwaua wanaume wawiliKatika kupiga jeki msako wao, DCI inatumia idara kadhaa za ujasusi kutoka kwa vitengo vya usalamaKangogo ndiye mshukiwa mkuu wa mauaji ya Konstebo John Ogweno mjini Nakuru na raia wa kawaida Peter Ndwiga
Kwa zaidi ya wiki moja sasa, bado koplo Caroline Kangogo yuko mbioni baada ya kufaulu kukwepa mitego kadhaa ya polisi.
Huku akiendelea kusakwa, Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) sasa inasema ni vigumu kumfuatilia afisa huyo wa polisi kwa sababu hatumii tena simu yake.
Hivyo, DCI na idara zingine za usalama zimeamua kumsaka Caroline Kangogo ambaye anatuhumiwa kuwaua wanaume wawili.
"Imekuwa changamoto kumfuatilia afisa huyo kwa sababu hatumii tena simu yake. Hata hivyo kikosi chetu kimehimarisha msako wake," alisema Afisa Mkuu wa Upelelezi kaunti ya Nakuru, Anthony Sunguti.
Read also
Baringo: Chatu Mkubwa Atembelea Kaburi la Mshikaji Nyoka Kumuomboleza
Kangogo ndiye mshukiwa mkuu wa mauaji ya Konstebo John Ogweno mjini Nakuru na raia wa kawaida Peter Ndwiga mjini Thika ambao walikutana na mauti yao chini ya saa 24.
Wahimarisha msakoKatika kupiga jeki msako wao, DCI inatumia idara kadhaa za ujasusi kutoka kwa vitengo vya usalama
Kikosi hicho ni ikiwemo polisi, jeshi na wengine kutoka idara za ujasusi.
Huku akikosa kupatikana kwenye simu, kikosi hicho kitafanya uchunguzi kwenye barabara kuu ikiwemo Nairobi-Nakuru-Eldoret na Nairobi kuelekea Mombasa.
Pia timu hiyo itafanya msako kwenye mahoteli, lojini na maeneo mengine ambazo mshukiwa anadaiwa kujificha.
Asafiri kaunti sitaRipoti za awali zilidai kwamba simu ya mshukiwa ilionyesha alitembea kaunti sita na wapelelezi wanaamini alikuwa anatumia magari ya umma akiwa amejiicha uso.
Mnamo Jumatano, Julai 7, simu yake ilifuatiliwa hadi Kahawa Wendani, Nairobi mwendo wa saa nane asubuhi na siku hiyo alifika Kericho ambapo anaaminika kumpigia mtu simu akitumia simu ya kuomba.
Read also
Mzee wa Legio Maria Aliyetabiri Ajali ya Homabay Miongoni Mwa Wahanga
Kisha Kangogo alisafiri hadi kaunti za Kisii, Iten, Elgeyo Marakwet ambapo pia ni nyumbani kwao.
Mnamo Alhamisi, Julai 8, simu yake ilionyesha alikuwa eneo la Kenlands, kaunti ya Nakuru mwendo wa saa tisa asubuhi na saa 12 baadaye alionekana mara ya mwisho Eldoret.
Baada ya mauaji ya Juja, koplo huyo alitoa KSh 20,000 kutoka kwa kaunti yake na KSh 40,000 kutoka kwa akaunti yake ya Sacco ya polisi.
Anakwepa mitego ya polisi kwa kuzima simu yake ili kuwapofusha kuhusu hatua zake.
READ ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.