Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Caroline Kangogo: Makachero waanza kutatua kitendawili kuhusu kifo cha polisi

516a99849ccf4f7a Caroline Kangogo: Makachero waanza kutatua kitendawili kuhusu kifo cha polisi

Fri, 16 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kangogo anasemekana alikatiza maisha yake baada ya kujipiga risasi bomani kwao Elgeyo Marakwet Ijumaa, Julai 16 asubuhiMakachero wamepiga kambi katika eneo ambapo mwili kwake ulipatikana ili kutegua kitendawili kuhusiana na kifo chakeMwili wa afisa huyo ulipatikana katika bafu ambapo alisemekana alijitia kitanziMaafisa wa idara mbai mbali wameanzisha uchunguzi ili kutatua kitendawili kuhusiana na kifo cha afisa wa polisi Caroline Kangogo.

Kangogo anasemekana alikatiza maisha yake baada ya kujipiga risasi bomani kwao Elgeyo Marakwet Ijumaa, Julai 16 asubuhi.

TUKO.co.ke imebaini kwamba wapelelezi wamepiga kambi katika eneo ambapo mwili kwake ulipatikana ili kutegua kitendawili kuhusiana na kifo chake.

Mwili wa afisa huyo ulipatikana katika bafu ambapo alisemekana alijitia kitanzi.

Picha zilizosambazwa mitandaoni zilimuonyesha Kangogo akiwa ameketi chini na bastola aina ya Ceska ambayo anadaiwa kutumia ikiwa katika mkono wake wakulia.

Picha hizo zilizua shauku miongoni mwa wengi huku baadhi wakihisi huenda afisa huyo aliuawa.

Seneta wa Makueni Mutula Kilonzo alikuwa mmoja wa Wakenya waliotoa hisia zao kuhusiana na eneo alikopatiakana Kangogo.



Read also

Mwili wa Konstebo Caroline Kagongo Kuhifadhiwa Katika Makafani ya Hospitali ya Eten

"Picha ya eneo ambalo polisi mtoro anadaiwa kujipiga risasi ni nadhifu sana - hata ameketi ni kana kwamba alikuwa akitazama televisheni, kisha tena bastola iko mikononi mwake," ujumbe wake ulisema.

Macho yote sasa yameelekezewa maafisa wa upelelezi ili waweze kutatua kitendawili cha kifo cha afisa huyo mtoro.

Kangogo alikuwa mshukiwa mkuu wa mauaji ya Konstabo wa Polisi John Ogweno, mjini Nakuru na Peter Njiru Ndwiga ambaye alikuwa mfanyabiashara wa eneo la Juja, Kiambu.

Kwa zaidi ya wiki moja sasa, afisa huyo wa kike, ambaye ametajwa kuwa mlenga shabaha stadi, alikuwa akisakwa na alikuwa amefanikiwa kukwepa mitego kadhaa ya polisi.

Maafisa wa polisi wa vitengo tofauti walikuwa wameunda kokosi ambacho kilikuwa kikifuata nyayo zake taratibu.

Afisa huyo imedaiwa alifika nyumbani kwao mwendo wa 5am na alijiua 7am.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.



Read also

Caroline Kangogo: Kifo cha Afisa Mtoro Chaibua Maswali Chungu Nzima

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke