Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

COVID-19: Watu 284 wanasa virusi huku wagonjwa 17 wakiangamizwa

46767d0d456f2228 COVID-19: Watu 284 wanasa virusi huku wagonjwa 17 wakiangamizwa

Fri, 4 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Jumla ya wagonjwa nchini imefika 171,942 huku asilimia mpya ya maambukizi ikigonga 6.3%

- Vifo vipya vilivyorekodiwa vilitokea kati ya mwezi wa Aprili na Mei

Mnamo Ijumaa, Juni 4 Kenya ilirekodi visa vipya 284 vya Covid-19, na kufikisha jumla ya wagonjwa nchini hadi 171, 942 Waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema.

Waziri Kagwe katika taarifa yake alithibitisha kuwa idadi hiyo ya wagonjwa ilitokana na sampuli 4,540 zilizopimwa katika saa 24 ambapo kiwango cha maambukizi ni asilimia 6.3 %.

Jumla ya vipimo tangu kisa cha kwanza kutua Kenya mwezi Machi 2020 imefika 1,826,756.

Katika visa vipya Wakenya ni 272 na 12 raia wa kigeni.

Idadi ya waliofariki dunia kufikia sasa kutokana na maradhi hayo hatari imefika 3,240 baada ya wagonjwa wengine 17 kupoteza maisha yao kati ya mwezi wa Aprili na Mei.

Kagwe alisema wagonjwa 1,207 wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya kote nchini na wengine 4,957 wanahudumiwa wakiwa makwao.

Jumla ya wagonjwa 102 nao wamelazwa katika hali mahututi.

Wakati uo huo, wagonjwa 306 wameripotiwa kupata nafuu, 217 kati yao walikuwa wakipokea matibabu manyumbani mwao nao 89 walikuwa wakiunguzwa katika hospitali tofauti tofauti nchini.

Jumla ya wagonjwa 96 nao wamelazwa katika hali mahututi.

Wakati uo huo, wagonjwa 124 wameripotiwa kupata nafuu, 27 kati yao walikuwa wakipokea matibabu manyumbani mwao nao 97 walikuwa wakiunguzwa katika hospitali tofauti tofauti nchini.

Jumla ya wagonjwa waliopona imaefika 117,469 ambapo 85,291 kati yao walikuwa wkaihudumiwa nyumbai nao 32,178 walipata matibabu katika vituo mbali mbali vya afya nchini.

Idadi ya maambukizi ilirekodiwa kama ifuatavyo katika kaunti;

Siaya na Nairobi visa 66 kila moja, Kisumu 30, Mombasa 21, Busia 13, Kericho na Nyeri visa 8 kila moja, Kiambu, Nakuru, Turkana na Uasin Gishu visa 7 kila moja.

Garissa na Vihiga visa 6 kila moja, Kisii 5, Murang’a 4, Kitui 3, Embu, Migori, Kakamega, Narok, Kirinyaga na Kwale visa 2 kila moja.

Lamu, Marsabit, Meru, Nandi, Trans Nzoia, West Pokot, Homa Bay na Kajiado kisa kimoja kila kaunti.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke