Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

COVID-19: Wagonjwa 18 Waripotiwa Kufariki Dunia, 141 waingia ICU

84cfc7acc34eb8ea COVID-19: Wagonjwa 18 Waripotiwa Kufariki Dunia, 141 waingia ICU

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Idadi ya vifo nchini Kenya tangu Machi 2020 sasa imefikia 2,066

- Wagonjwa 141 wamelazwa ICU

- Jumla ya wagonjwa waliopata nafuu nchini imefika Kenya imefika 90,770

Kenya ilirekodi visa vingine 1,540 vipya vya Covid-19, na kufikisha idadi ya maambukizi nchini kugonga 124,707 Wizara ya Afya ilisema.

Katika taarifa yake, Katibu wa Wizara ya Afya Mercy Mwangangi alisema idadi hiyo alithibitisha kutokana na sampuli ya 9,348 kupimwa katika saa 24 zilizopita.

Idadi ya sampuli zilizopimwa kufikia sasa ni 1,425,377.

Idadi ya vifo nayo pia imeongezeka hadi 2,066 baada ya wagonjwa wengine kumi na wanane kuangamizwa na makali ya maradhi hayo.

Mwangangi alisema kuwa kuna wagonjwa 1,073 waliolazwa katika hospitali mbali mbali nchini. Wengine 3,315 wanapokea huduma wakiwa nyumbani.

Jumla ya wagonjwa 141 wako hali mahututi, 99 ​​kati yao wanaoongezewa oksijeni.

Wakati huo huo, wagonjwa 184 wameripotiwa kupata nafuu, 89 kati yao wakihudumiwa hospitalini na 95 manyumbani mwao.

Jumla ya waliopata nafuu nchini imefika 90,770. Kati ya visa vilivyorekodiwa Jumanne watu 1,446 ni Wakenya wakati 94 ni raia wa kigeni.

Kwa upande wa jinsia, wanaume ni 829 nao 711 ni wanawake na mgonjwa mwenye umri mdogo ni mtoto wa miezi sita na mkongwe ana miaka 110.

Katibu huyo aliwataka Wakenya kuzingatia kanuni zilizotangazwa na serikali kujikinga ikiwa ni pamoja na; kunawa mikono, kujiepusha na mirundikano ya watu na vile vile kuvalia maski ifaavyo.

"Tumeona watu wakilegeza masharti ya kudhibiti maabukizi ya Covid-19, jambo ambalo linasikitisha mno kwa sababu hospitali zetu zimefurika wagonjwa hata wengine wamekosa vitanda," alisema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke