Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

COVID-19: Rais Uhuru Kenyatta aongeza lockdown kwa siku 60

C7404518c8886068 Rais Uhuru Kenyatta

Wed, 18 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta ameongeza muda wa kutokuwa nje kuanzia saa nne usiku hadi saa kumi alfariki kwa siku 6.

Hii ni baada ya Rais kufanya mkutano na viongozi wa upinzani pamoja na waziri wa afya Mutahi Kagwe hii leo Jumatano, Agosti 18.

Uhuru alisema hatua hii inanua kuzuia na kudhibiti maambukizi zaidi ya virusi vya COVID-19 ambapo kufikia Jumatano, Agosti 18 vifo 4,378 kwa jumla vilikuwa vimeripotiwa na visa 224,400 vikirekodiwa.

Rais alipiga marufuku mikusanyika mikubwa ikiwemo ya kisiasa akiwaomba Wakenya wawe watulivu serikali ikitafuta mbinu mwafaka ya kupunguza maambukizi.

Watu wasiopita 100 ndio wataruhusiwa kwenye mikusanyika kama ya harusi, hafla za mazishi na sherehe zingine zile, watakaokiuka amri hii watakabiliwa kisheria.

" Kaunti nyingi zimerekodi asilimia kubwa ya viwango vya maambukizi, kwa muda wa wiki moja iliyopita pekee kaunti zilirekodi viwango vya zaidi ya asilimia 30%, Kiambu, Nyandarua, Murang’a, Makueni, Machakos, Baringo, Meru na Nyeri zikiongoza," Uhuru alisema.

Hata hivyo,Wakenya wanaonekana kughadhabishwa na uamuzi wa serikali na wengi wameelezea hisia zao mitandaoni. Soma baadhi ya maoni yao;

Ja Loka@_fels1 alisema;

Hii ni upuzi gani, Matatu inajaza abiria, mikutano ya kisiasa inaendelea kama kawaida, makanisa yamejaa lakini nikama corona inapatika usiku pekee."

MK@Baby_martinkk alisema;

" Mbona siku 60 za kafyu na kila Mkenya anakimbilia kupata chanjo katika vituo vya karibu vya afya, tumeanza kuzoea hali ilivyo, maliza kafyu tuendelee na maisha ya kawaida."

Fleur-de-lisANCIENT SOULFleur-de-lis@ancientsou1

Ule Mkenya ambaye anadhani kafyu ni ya Covid...umelala darasani

Mnazoeashwa authoritarianism mpaka mkuwe compliant,"

Nchi kwa jumla imerekodi visa 224,400 na sampo zilizofanyiwa vipimo ni 2,278,763.

Kwa mujibu wa wizara ya afya, kufikia Agosti 17, jumla ya watu 2,154,825 walikuwa wamepokea chanjo za kuzuia virusi hivyo.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke