Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

COVID-19:Rais Museveni atangaza Ijumaa, Juni 25, kuwa siku ya Maombi Uganda

Db317867d1ba607a COVID-19:Rais Museveni atangaza Ijumaa, Juni 25, kuwa siku ya Maombi Uganda

Fri, 25 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kufikia sasa Uganda imerekodi visa 74, 260 vya maambukizi ya virusi vya covid-19 na vifo 752 tangu mwezi Machi mwaka wa 2020Rais Yoweri Museveni ametangaza siku ya Ijumaa, Juni 25 kuwa siku ya maombi na ya mapumziko kwa nchi hiyoMuseveni amewarai wananchi kuombea wataalamu wa afya na familia zilizoathirika na ugonjwa huoViongozi wa makanisa watafanya maombi yao kupitia mtandao wa ZoomRais wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza Ijumaa, Juni 25 kuwa siku ya maombi kufuatia ongezeko la vifo na maambukizi ya virusi vya COVID-19.

Museveni alisema siku hiyo pia itakuwa ya mapumziko kwa taifa hilo.

Kufikia sasa nchi hiyo imerekodi visa 74, 260 vya maambukizi ya virusi hivyo na vifo 752 tangu mwezi Machi mwaka wa 2020.

" Rais ametumia mamlaka yake chini ya kifungu cha 2 (2) kutangaza Ijumaa, Juni 25 kuwa siku ya mapumziko ili kuwawezesha wananchi kumuomba Mungu kuingilia kati kuwaepusha na janga la ugonjwa wa COVID-19.Taarifa kutoka ikulu ya Uganda ilisoma.

Viongozi wa makanisa mbali mbali watafanya maombi yao kupitia mtandao wa Zoom ikiwa ni njia moja ya kuepuka mikusanyiko na mikutano ambayo itaweza kuchangia ongezeko la maambukizi.

Rais Museveni amewaomba raia wote wa Uganda kuwaombea wataalamu wa afya na familia ambazo zimeathirika na ugonjwa huo.

Taarifa hii inajiri huku Museveni akiwa amefunga nchi kwa siku 42 baada ya vifo 42 kuripotiwa nchini humo na maambukizi 1,000 kurekodiwa kwa muda wa siku moja.

Museveni pia alitangaza kufungwa kwa shule zote kwa siku 42, aliwahimiza walimu wapokee chanjo ya kudhibiti makali ya virusi hivyo kabla ya kurejea shuleni.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke