Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

COVID-19: Kenya yarekodi maambukizi mapya 433, maafa 18

COVID COVID-19: Kenya yarekodi maambukizi mapya 433, maafa 18

Wed, 9 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

-Idadi ya watu waliopoteza maisha yao kutokana na makali ya virusi vya corona imefika 3,326 baada ya wagonjwa wengine 18 kuaga dunia

- Wagonjwa 1,125 wamelazwa katika hospitali mbali mbali kote nchini, wengine 4,895 wanapokea huduma za matibabu wakiwa manyumbani wao

- Waziri Kagwe alithibitisha kuwa idadi hiyo ilirekodiwa kutokana na sampuli 4,479 zilizopimwa na kuonesha kuwa asilimia mpya ya maambukizi ni 9.7

Mnamo Jumanne, Juni 8 Kenya ilirekodi visa vpoya 433 vya Covid-19, na kufikisha idadi ya wagonjwa nchini kufikia 173,072, Waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema.

Katika taarifa yake, Kagwe alithibitisha kuwa idadi hiyo ilirekodiwa kutokana na sampuli 4,479 zilizopimwa na kuonesha kuwa asilimia mpya ya maambukizi ni 9.7

Idadi ya sampuli zilizopimwa tangu kisa cha kwanza cha coronavirus kutua nchini mnamo mwezi Machi 2020 imefika 1,840,889.

Idadi ya watu waliopoteza maisha yao kutokana na makali ya virusi vya corona imefika 3,326 baada ya wagonjwa wengine 18 kuaga dunia.

Kagwe alisema kuwa kuna wagonjwa 1,125 waliolazwa kwa sasa katika hospitali mbali mbali kote nchini. Wagonjwa wengine 4,895 wanapokea huduma za matibabu wakiwa manyumbani wao.

Jumla ya wagonjwa 111wamelazwa wakiwa hali mahututi.

Wakati uo huo, wagonjwa 395 wameripotiwa 395 kupona ambapo 262 kati yao walikuwa wakihudumiwa nyumbani nao 133 kutoka vituo mbali mbali vya afya.

Jumla ya wagonjwa waliopata nafuu sasa imegonga 118,621.

Aidha waziri huyo alisema kufikia sasa watu 1005,509 wamepokea chanjo nchi nzima. Kati ya yao, 27,382 wamepokea dozi zao za pili.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke