Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

COVID-19: Idadi ya Maambukizi Kenya Yatimia 153,488

20a148da866a37e4 COVID-19: Sudan Kusini yaharibu chanjo 60,000 za aina ya AstraZenica

Wed, 21 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Watu 965 wameambukizwa Covid-19 katika saa 24 zilizopita kutoka kwa sampuli 7,311 zilizopimwa.

Idadi ya watu walioambukizwa Covid-19 nchini Kenya sasa ni 153,488. Tangu Machi jumla ya sampuli zilizopimwa imefika 1,618,990

Kati ya visa vilivyotangazwa leo, wagonjwa 907 ni Wakenya nao 58 ni wageni. Wagonjwa 560 ni wa kiume na 405 ni wa kike.

Mgonjwa mwenye umri wa mdogo ni mtoto wa miezi mitatu naye mkongwe zaidi akiwa na miaka .

Aidha watu 21 waliripotiwa kuaga dunia ambapo jumla ya waliopoteza maisha yao kutokana na makali ya coronavirus imefika 2540.

Wakati huo huo, wagonjwa 1,441 waliripotiwa kupata nafuu 1,371 kati yao walikuwa wakihudumiwa nyumbani wakati 124 nao walikuwa wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya.

Idadi ya waliopata nafuu imegonga 105,279. Kati ya waliopona, wagonjwa 76,967 walikuwa wakihudumiwa nyumbani mwao nao watu 28,312 walikuwa katika vituo mbali mbali vya afya nchini.

Jumla ya wagonjwa 1,509 kwa sasa wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya nchini kote, wakati wagonjwa 6,808 wametengwa manyumbani mwao.

Wagonjwa 240 wako katika Kitengo cha Huduma Mahututi (ICU), 151 nao wanaongezewa oksijeni.

Idadi ya maambukizi ni kama ifuatavyo;

Nairobi 330, Mombasa 67, Nakuru 63, Kericho 45, Uasin Gishu 44, Murang’a 33, Kiambu 30, Meru 28, Homa Bay 25, Kisumu 25, Garissa 22, Isiolo 20, Nyeri 19, Laikipia na Siaya visa 17, Narok na Busia visa 14 kila moja, Kajiado 13, Machakos 12.

Kisii na Embu visa 11, Makueni, Bungoma, Nyandarua na Kilifi visa 10, Kitui 9, Kakamega 8, Mandera na Migori visa 7, Bomet 6, Taita Taveta 5, Nandi, Turkana na Samburu visa 4 kila moja, Kirinyaga na Trans Nzoia visa 3 kila moja, Baringo na West Pokot visa 2 nayo Vihiga kisa kimoja.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke