Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

COVID-19: Asimilia mpya ya maambukizi ni 8.9, wagonjwa 17 waangamia

060381478430e4d1 COVID-19: Asimilia mpya ya maambukizi ni 8.9, wagonjwa 17 waangamia

Sat, 29 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mnamo Jumamosi, Mei 29 Kenya ilirekodi visa vipya 444 vya Covid-19, na kufikisha jumla ya wagonjwa nchini hadi 170,485,Waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema.

Waziri Kagwe katika taarifa yake ilithibitisha kuwa idadi hiyo ya wagonjwa ilitokana na sampuli 4,989 zilizopimwa katika saa 24 ambapo kiwango cha maambukizi ni asilimia 8.9.

Jumla ya vipimo tangu kisa cha kwanza kutua Kenya mmwezi Machi 2020 imefika 1,806,438.

Idadi ya waliofariki dunia kufikia sasa kutokana na maradhi hayo hatari imefika 3,141 baada ya wagonjwa wengine 17 kupoteza maisha yao.

Kagwe alisema wagonjwa 1,171 wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya kote nchini na wengine 4,682 wanahudumiwa wakiwa makwao.

Jumla ya wagonjwa 104 nao wamelazwa katika hali mahututi.

Wakati uo huo, wagonjwa 115 wameripotiwa kuapa nafuu, 76 kati yao walikuwa wakipokea matibabu manyumbani mwao nao 39 walikuwa wakiunguzwa katika hospitali tofauti tofauti nchini.

Jumla ya waliopata nafuu sasa imefika 116,133, ambapi 84,426 kati yao walihudumiwa manyumbani nao 31,707 walikuwa katika hospitali mbali mbali nchini.

Katika visa vipya vilivyoripotiwa Jumamosi, 435 ni Wakenya wakati 9 ni wageni. 259 ni wanaume na 185 wanawake. Mgonjwa mdogo ni mtoto wa miezi miwili wnaye mkongwe ana miaka 101.

Kwa upande wa chanjo, jumla ya watu 968,733 hadi sasa wamepatiwa chanjo dhidi ya ugonjwa wa COVID-19 nchi nzima.

Visa hivyo vilrekodiwa kama ifuatavyo katika kaunti; Nairobi 54, Siaya 53, Busia 47, Kisumu 43, Kisii 41, Kakamega 31, Kericho 24, Mombasa 21, Bungoma 15, Homa Bay 13, Kilifi 9, Nyamira 9, Kitui 9.

Uasin Gishu 8, Nakuru 7, Migori 7, Baringo 5, Murang’a 5, Trans Nzoia 5, Bomet 5, Kiambu 4, Kirinyaga 4, Machakos 4, Nyeri 4, Nandi 3,Tharaka Nithi 2, Embu 2, Meru 2, West Pokot 2, Narok 2, Nyandarua 1, Laikipia 1 na Makueni 1.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke