Tue, 27 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Burundi imeinyoshea kidole Rwanda kuhusika katika Shambulio ambalo lilipelekea watu tisa kuuawa katika mkoa wa Bubanza Magharibi mwa Burundi kwa kuwafadhili waasi.
Hata hivyo, waasi wa Red Tabara wanakanusha taarifa za kufadhiliwa na Serikali ya Rais Paul Kagame.
Miongoni mwa waliouawa katika shambulio hilo ni pamoja na Wanawake sita waliokuwa msibani,askari mmoja wa Jeshi la Burundi huku watano wakijeruhiwa wakiwemo Wanawake watatu.
Januari, 2024 Burundi ilichukuwa hatua ya kuifunga mipaka yake na Rwanda ikiishutumu kuwaficha waasi wa Red Tabara.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live