Fri, 19 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Burkina Faso imewafukuza Wanadiplomasia watatu wa Ufaransa ikiwashutumu kuhusika katika uvunjifu wa amani kama ambavyo imetangazwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo.
Wafanya kazi hao wa Ubalozi wa Ufaransa wakiwemo washauri wawili katika mambo ya siasa wamepewa saa 48 kuondoka nchini Burkina Faso.
Uhusiano kati ya Burkina Faso na Ufaransa ambayo iliwahi kuiongoza nchi hiyo wakati wa ukoloni uliingia doa baada ya Kapteni Ibrahim Traore kuingia madakani mwaka wa 2022 kwa njia ya Mapinduzi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live