Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bunge la kitaifa kuamua ustahiki wa Jaji Mkuu Mteule Martha Koome

286669b133712aa8 Bunge la kitaifa kuamua ustahiki wa Jaji Mkuu Mteule Martha Koome

Tue, 18 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Bunge la Kitaifa litafanya kikao maalum ili kutoa ripoti ya Kamati ya Haki na Maswala ya Sheria kuhusiana na uteuzi wa Koome

- Kamati hiyo ilimchunguza jaji huyo wa mahakama ya rufaa ambaye anataka kuwa Jaji Mkuu wa kwanza mwanamke mnamo Alhamisi, Mei 13

- Atateuliwa rasmi na Rais Uhuru Kenyatta ikiwa bunge litaidhinisha uteuzi wake

Jaji Mkuu mteule Martha Koome atajua hatma yake mnamo Jumatano, Mei 19 wakati Bunge la Kitaifa litajadili kuhusu ustahiki wake kabla ya kuanza kazi rasmi.

Spika wa Bunge la Kitaifa Justin Muturi, katika chapisho la gazeti, alisema Bunge litaitisha kikao maalum ili kutoa ripoti ya Kamati ya Sheria na Maswala ya Sheria kuhusu uteuzi wa Koome.

Mnamo Alhamisi, Mei 13, kamati ilimchunguza jaji huyo wa rufaa ambaye anataka kuwa jaji mkuu wa kwanza mwanamke katika historia ya mahakama ya Kenya.

Ikiwa bunge litaidhinisha uteuzi wa Koome, basi atateuliwa rasmi na rais.

Jaji huyo alichanguliwa kutoka kwa wagombea wengine 10 waliokuwa wametuma maombi yao kwa kamati ya Tume ya Usimamizi wa Mahakama (JSC) iliyoongozwa na mwenyekiti Olive Mugenda.

Koome alianza taaluma yake ya sheria baada ya kujiunga na Kaouni ya Mathenge and Muchemi Advocates, ambapo alihudumu kama Jaji wa Mahakama Kuu kati ya 2003 na 2011.

Wakati ambao aliongoza Idara ya Mazingira na Ardhi jijini Nairobi. Alikuwa pia jaji mkazi huko Kitale na Nakuru.

Mnamo mwaka wa 2012, Koome alipandishwa cheo hadi kwa Mahakama ya Rufaa Nairobi, Nyeri, na Malindi. Wenzake walimchagua kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mahakimu na Majaji wa Kenya.

Wakati wa mahojiano, aliliambia jopo kwamba la JSC alipata shahada ya kwanza mnamo 1985 na uzamili katika Sheria ya Umma ya Kimataifa mnamo 2010 kutoka Chuo Kikuu cha London.

"Nililelewa vijijini huko Meru, kwa hivyo mimi ni mwanakijiji halisi. Wazazi wangu walikuwa wakulima na masikini, na sisi tulikuwa watoto 18 kutoka kwa mama wawili, "alisema.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke