Wed, 2 Mar 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari tayari ameondoka Jijini Abuja Machi Mosi kuelekea Kenya kushiriki katika Bunge la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEA) na kuadhimisha miaka 50 ya Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa (Unep).
Mkutano huo wa UNEA, amabo ulianza Jumatatu, unatarajiwa kujadili mabadiliko ya hali ya hewa, bioanuwai na upotevu wa asili, pamoja na udhibiti wa taka na uchafuzi wa mazingira.
Rais Buhari, 78, atakuwa Nairobi kwa siku nne kabla ya kuelekea London kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live