Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bonface Mwangi aashiria jamaa wa Kite walimalizwa na kikosi spesheli cha polisi

25fa9601656e7c15 Bonface Mwangi aashiria jamaa wa Kite walimalizwa na kikosi spesheli cha polisi

Fri, 30 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mwangi anatamani kukutana na kikosi kilichowamaliza ndume wanne kutoka Kitengela

- Kulinagana naye, mauaji hayo yalifanywa na kikosi cha 'hit squad' ambacho kilizungumziwa mtandaoni

- Miili ya watatu kati ya jamaa hao wanne imekwisha patikana ikiwa imetupwa mtoni

Mwanaharakati Bonface Mwangi ameashiria kuwa jamaa wanne kutoka Kitengela walimazwa na kikosi spesheli cha polisi.

Wanne hao wamekuwa wakitafutwa tangu Jumapili Aprili 19 na tayari miili ya watatu imepatikana ikiwa imetupwa maeneo ya Murang'a, Thika na Mathioya.

Kupitia kwa ukurasa wake wa Facebook, Mwangi alisema kikosi hicho alichoita 'Hit squad' kiliwawekea mtego ndume hao na kuwaangamiza.

"Kikosi cha polisi cha kumaliza watu kiliwalenga washukiwa wanne wa ujambazi na kuwamaliza," alisema Mwangi.

Mwangi pia alichapisha ujumbe wa akaunti ya mwanamtandao anayejiita Blackest Widow ambaye alianika anachokijua kuhusu wanne hao.

Kupitia kwa akaunti hiyo, mwanamtandao huyo aliwataka Wakenya kutoomboleza vifo vyao kwa kuwa waliwatesa wengi.

"Wakenya wapenda amani hawafai kuhurumia watu kama hawa. Hii kanairo lazima iwe crime free," ujumbe wa Backest Widow ulisema.

Mwanaharakati huyo alisema yuko tayari kukutana na kikosi hicho ili kujua mengi kuhusu kazi yao.

"Naomba kunywa chai na hii squad iko na code name za aajabu. Tukunywe Ketepa crew, bora msinizamishe, mimi si mkora. Ingieni DM, na msipige simu hii serikali yenyu inasoma na kuskiza kila kitu," alisema Mwangi.

Kumekuwa na ripoti kuwa huenda wanne hao walikuwa wakihusika na uhalifu wa hali ya juu na hivyo kuwindwa na makachero.

Hata hivyo, Inspekta jenerali wa polisi Hillary Mutyambai alisema ameunda kikosi spesheli cha kuchunguza waliohusika na mauaji hayo.

Familia za jamaa hao zimeililia serikali kuchunguzi waliohusika na wakisema jamaa wao walikuwa ni wangwana waliojitafutia riziki kwa njia za haki.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke