Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bomu lililotegwa katika mkokoteni wa punda laua afisa wa polisi wa Kenya

Bomu Lililotegwa Katika Mkokoteni Wa Punda Laua Afisa Wa Polisi Wa Kenya.jpeg Bomu lililotegwa katika mkokoteni wa punda laua afisa wa polisi wa Kenya

Thu, 18 Jan 2024 Chanzo: Bbc

Bomu lililokuwa limefungwa kwenye mkokoteni wa punda limeripuka kwenye mpaka wa Kenya na Somalia na kumuua afisa mmoja wa polisi, vyombo vya habari vya ndani vinaripoti.

Watu wengine wawili walijeruhiwa, kulingana na chapisho kwenye mtandao wa X kutoka gazeti la Nation.

Inasemekana kwamba punda hao wawili waliokuwa wakivuta mkokoteni walinusurika.

Maafisa wa polisi walikuwa wakikagua bidhaa zilizokuwa nyuma ya toroli baada tu ya kuvuka hadi Kenya katika eneo la Mandera, ambalo liko kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo, wakati bomu lilipolipuka, ripoti zinasema.

Video inayosemekana kutoka eneo la tukio inaonyesha moshi mkubwa mweusi ukifuka kutoka mahali ambapo mlipuko huo ulitokea. Picha za matokeo zinaonyesha punda aliyejeruhiwa akiwa amesimama.

Mandera hapo imekuwa ikilengwa na kundi la wanajihadi la al-Shabab lenye makao yake nchini Somalia.

Chanzo: Bbc