Sat, 17 Dec 2022
Chanzo: Bbc
Mkuu wa kituo cha utamaduni wa Urusi katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati amejeruhiwa kwa bomu la kifurushi.
Ubalozi wa Urusi umesema amejeruhiwa kichwani na anapata matibabu katika hospitali katika mji mkuu, Bangui.
Kikundi cha mamluki cha Urusi Wagner kiliilaumu Ufaransa kwa tukio hilo, likiishutumu kwa kudhamini ugaidi.
Kikundi cha Wagner kinaendesha harakati zake katika nchi kadhaa za Afrika zikiwemo Mali na Jamuhuri ya Afrika ya Kati.
Chanzo: Bbc