Wed, 4 Sep 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii na Kiongozi wa Upinzani nchini Uganda, Boby Wine, amepigwa risasi ya miguu akiwa katika hali ya vuta nikuvute na Polisi katika kijiji cha Bulindo nchini Uganda.
Kiongozi huyo ambaye ni mwanasiasa amekimbizwa hospitalini kwa ajili ya matibabu zaidi.
Kupitia mtandao wa kijamii wa X,Mwendesha ukarasa wa mtandao wa Boby Wine ametangaza kuwa Polisi walimpiga msanii huyo risasi ya mguu.
Hadi kufikia sasa hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na Jeshi Polisi kuhusu tukio hilo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live