Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Betty Barasa: Polisi wanasema mauaji ya mwanahabari yalipangwa

C4bc6086e391aa54 Betty Barasa: Polisi wanasema mauaji ya mwanahabari yalipangwa

Sat, 10 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Maafisa wa upelelezi wamesema wamepata magwanda ya risasi ambayo itafanyiwa uchunguzi wa kina

- Hilo litawasaidia kuwanasa washukiwa ambao wangali mafichoni

- Wapelelezi walisema majangili walionekana kumlenga Betty Barasa kati ya watu wengine sita ambao pia walikuwa katika nyumba hiyo

Wapelelezi wanaochunguza kifo cha mhariri wa video wa KBC aliyeuawa Betty Barasa sasa wanaamini kwamba mauaji yake yalipangwa.

Wapelelezi walisema washambuliaji walionekana kumlenga yeye kati ya watu wengine sita ambao pia walikuwa ndani ya nyumba hiyo, pamoja na rafiki yake.

Duru ziliarifu Citizen TV kwamba, wapelelezi wanaoshughulikia kesi hiyo sasa wanaipekua kwa kina hususan kuhusu kupangwa kwa mauaji ya mwanahabari huyo.

Makachero pia walisema walipata gwanda la risasi ambalo kwa sasa wanalikagua ili kuwanasa washukkiwa ambao wangali mafichoni.

"Tunachoahidi ni kwamba tunafanya uchunguzi kwa kina, na kwa sasa tunaendelea vizuri, na kutakuwa na mafanikio," Kamanda wa Polisi Patrick Manyasi alisema.

Kulingana na uchunguzi wa upasuaji wa maiti yake, Betty aliaga dunia baada ya kupigwa risasi moja kichwani.

Mumewe Geoffrey Barasa alisema majangili waliomupiga risasi na kumuua Barasa walikuwa wamevalia nguo zito nzito na glavu.

"Wawili kati yao walikuwa na bunduki za aina ya AK47 na mmoja wao alikuwa na G3. Walikuwa wamevalia glavu nzito na vile vile walifunika nyuso zao na maski," aliwaambia waandishi wa habari.

"Walituamuru tulale chini. Waliitisha pesa," aliongeza.

Simu ya rununu ambayo ilikuwa imeibwa kwa Betty ilipaikana katika boma lao mnamo Alhamisi.

Alisema mmoja wa majangili alipiga simu ya kutatanisha ya kusema amemaliza kazi.

Wafanyikazi wenza wa Betty ambao wangali na mshtuko kufuatia kifo chake cha ghafla walimtaja Betty kama mtu aliyependa kutabasamu na ambaye alisalia mtulivu siku ya tukio.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke