Wed, 20 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Benki ya Biashara nchini Ethiopia (CBE) imetoa wiki moja kwa wateja waliotoa pesa zaidi ya walizokuwa nazo kwenye akaunti zao baada ya kutokea kwa hitilafu wazirudishe, vinginevyo watakamatwa na kufunguliwa mashtaka.
Rais wa CBE, Abe Sano amesema baadhi ya wateja waliotoa pesa za ziada tayari wamezirudisha.
Zaidi ya TZS bilioni 102 zimeripotiwa kutolewa kwenye benki hiyo inayomilikiwa na Serikali, huku pesa nyingine zikiripotiwa kuhamishiwa kwenye benki nyingine.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live