Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Benjamin Ayimba: Mkongwe wa raga yupo hali mahututi baada ya kunasa maleria kali

0fgjhs3cf95k0feee Benjamin Ayimba: Mkongwe wa raga yupo hali mahututi baada ya kunasa maleria kali

Fri, 9 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Kulingana na familia, Ayimba amekuwa akiugua kipindi kirefu cha kuanzia 2021, na hali hiyo inamfanya asiweze kujitokeza kwa umma

- Inaeleweka kuwa bingwa huyo wa zamani wa Shujaa Sevens kwa sasa amelazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi cha Nairobi Hospital

- Familia ilifichua kuwa Ayimba anahitaji matibabu maalum katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta

- Walakini, wanahitaji kwanza kulipia bili kubwa ya matibabu ya zaidi ya KSh 2.2 milioni ili uhamisho wake ufanyike

- Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 43 anakumbukwa sana kwa mafanikio yake akiwa kocha mkuu wa Kenya Sevens aliposaidia timu hiyo kushinda Msururu wa IRB Sevens huko Singapore miaka minne iliyopita

Sogora wa mchezo wa raga nchini Kenya Benjamin Ayimba ameripotiwa kuwa katika hali mbaya kufuatia kugunduliwa kuwa na ugonjwa wa malaria ya ubongo.

Inafahamika amekuwa akipambana na hali hiyo kwa miezi kadhaa sasa, na hali hiyo imemzuia kutoonekana hadharani kwa umma tangu mwanzoni mwa mwaka huu.

Kulingana na The Standard ambalo lilinukuu vyanzo vya habari hii kutoka kwa familia, Ayimba kwa sasa amelazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (HDU) katika Nairobi Hospital, na hawezi kuzungumza au kumtambua mtu yeyote tokea siku kadhaa zilizopita.

"Haya yote wakati tumejaribu kudumisha faragha na hadhi yake lakini imefikia mahali ambapo hatuwezi kukaa kimya tena," familia iliiambia The Standard.



Kifungua mimba wa Ayimba, Brian, alifunguka zaidi kwamba mkongwe huyo wa raga anahitaji matibabu maalum, na familia imeombwa itoe kima cha KSh 2.2 milioni kabla ya kumhamisha.

“Familia ilidhani haingekuwa mbaya sana. Kwa hivyo, hatukutaka kuzua wasiwasi lakini wapi tumefika hapa sasa, tunatoa wito kwa wahisani wote nchi nzima kutusaidia," alisema.

"Kwa kuwa bili ya hospitali sasa ni zaidi ya Sh2.2 milioni, tunahitaji msaada kwani tumemaliza rasilimali za familia," akaongeza.

Ayimba anachukuliwa kuwa mkongwe wa raga ya Kenya, kutokana na mchango wake katika mchezo huo akiwa mchezaji na kocha.

Aliunda sehemu ya kikosi cha Kenya kilichocheza kwenye Kombe la Dunia la Rugby Sevens la 2001 na 2005.

Baadaye akawa kocha wa timu hiyo, akiwahimiza kwa ubingwa wakati wa safu ya 2016 IRB Sevens ya Singapore.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke