Thu, 14 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mamlaka ya Udhibiti wa Mafuta na Nishati nchini Kenya (EPRA) imetangaza kupunguza bei za Petroli, Dizeli, na Mafuta ya Taa.
Kulingana na taarifa iliyotolewa Alhamisi, bei ya Petrol itapungua kwa Ksh.7.21, Dizeli kwa Ksh.5.09 na Mafuta ya Taa kwa Ksh.4.49.
Kufuatia mpango huo mpya lita moja ya petroli jijini Nairobi itauzwa kwa Ksh.199.15, dizeli kwa Ksh.190.38 na Mafuta ya Taa kwa Ksh.188.74.
Bei hizo mpya zitaanza kutumika kuanzia saa sita usiku, Machi 15 hadi Aprili 14, 2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live