Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bei mpya ya mafuta Kenya kutangazwa leo - EPRA

Bei Mpya Ya Mafuta Kenya Kutangazwa Leo   EPRA Bei mpya ya mafuta Kenya kutangazwa leo - EPRA

Fri, 30 Jun 2023 Chanzo: Voa

Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Petroli (EPRA) nchini Kenya itatangaza hii leo bei mpya za mafuta.

Bei hizo mpya zinatokana na Kodi mpya ya Ongezeko la Thamani kwenye bidhaa za petroli, ambayo sasa itakuwa asilimia 16, kufuatia kupitishwa kwa Sheria ya Fedha, 2023.

"Mnamo tarehe 26 Juni 2023, Rais Dkt William Ruto alitia saini kuwa sheria Mswada wa Fedha wa 2023 wa kuwasilisha VAT ya asilimia 16 kwa bidhaa za petroli. Kwa hivyo, @EPRA_ leo tarehe 30 Juni 2023 itatoa bei iliyopitiwa ya mafuta ya petroli kulingana na mswada wa fedha wa 2023. ," EPRA ilisema katika notisi.

Hapo awali, bidhaa za Petroli zilitozwa asilimia 8 ya VAT.

Haya yanajiri takriban wiki mbili baada ya EPRA kutangaza bei mpya za mafuta kwa mwezi wa Juni-Julai. Mabadiliko ya bei yangeanza Juni 15 hadi Julai 14, 2023.

Mnamo Juni 14, Mamlaka ilitangaza kuwa bei ya petroli ilipungua kwa Sh0.66 hadi rejareja kwa Sh182.04, huku dizeli ikipunguzwa kwa Sh1.12 hadi 167.28 jijini Nairobi.

Hata hivyo, bei ya mafuta ya taa iliongezwa kwa Sh0.35 hadi rejareja kwa Sh161.48.

Huku kiwango kipya cha VAT kikianza kutekelezwa, bei ya petroli huenda ikauzwa kwa Sh196.60 jijini Nairobi, dizeli Sh180.66, na Mafuta ya taa kwa Sh174.39.

Chanzo: Voa