Wed, 18 Aug 2021
Chanzo: www.habarileo.co.tz
RAIS Samia Suluhu, amefanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Malawi Joyce Banda, Lilongwe nchini Malawi ambapo Banda alimpongeza Rais Samia kwa kuwa Rais wa kwanza Mwanamke nchini Tanzania.
Banda pia alitumia wasaa huo kumpa pole Rais Samia kufuatia msiba wa Hayati John Magufuli ambaye alifariki Machi 17 mwaka huu, katika Hospitali ya Mzena kutokana na tatizo la moyo.
Aidha Banda amemuahidi Rais Samia ushirikiano akiwa kama Rais Msatafu Mwanamke.
Kwa upande wa Rais Samia, amemshukuru Banda baada ya kuahidi na kuendeleza ushirikiano wa kindugu na wa kihistoria kati ya Tanzania na Malawi.
Chanzo: www.habarileo.co.tz