Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Babes Alijua Kuhusu Uhusiano Wangu na Karen Nyamu, Samidoh Asema

F704e2d107c8818c Babes Alijua Kuhusu Uhusiano Wangu na Karen Nyamu, Samidoh Asema

Wed, 14 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Samidoh amesema alifungua roho kwa mkewe baada ya kujua kuwa mambo yataharibika kuhusu uhusiano wake na Nyamu

- Wawili hao walikuwa wakila tunda la penzi nje ya ndoa kwa muda kiwango cha kujaliwa mtoto wa kiume

- Samidoh alisema ilimuuma sana kusaliti penzi la mkewe ambaye wamekuwa pamoja kwa miaka 10

Msanii maarufu wa nyimbo za Kikuyu Felix Muchoki maarufu kama Samidoh amesema mkewe alijua kuwa alikuwa akichovya asali nje.

Samidoh alijipata pabaya baada ya siri yake kufichuka walipokosana na mpenziwe wa siri na moto kuwaka mtandaoni.

Nyamu alichapisha picha na video za muda wao wa mapenzi pamoja kama ushahidi kuwa msanii huyo alikuwa ameonja tunda lake.

Kwenye mahojiano na Churchill Show, msanii huyo alisema anajutia kuingia kwenye bakuli la asali la Nyamu.



Alisema alikutana na mkewe Edday miaka kumi iliyopita walipokuwa katika shule ya upili na ni kosa sana kusaliti penzi lake.

"Kabla hata ya haya mambo kuja kwa umma, alikuwa tayari amejua kuyahusu. Ilikuwa imenisumbua sana kwa muda na ikafika mahali nikafungua roho," alisema Samidoh.

Alisema tatizo kubwa na Wakenya ni kuwa hushabikia sana mambo ambayo ni mabaya kuliko yale mazuri ndio sababu walimkaanga mtandaoni.



Alimshukuru mkewe akisema alisimama naye baada ya sakata hiyo wakati ambapo dunia ilikuwa imemgeuka.

"Wakati sakata hiyo ililipuka alinisaidia sana. Nilikuwa tayari nimemwambia na kumuomba msamaha. Lakini niliamua sitashinda kwenye suala hilo kwa sababu kuna watu hata walikataa kuamini niliyoyasema," alisema Samidoh.

Kulingana na Nyamu, Samidoh alikuwa amempa matumaini ya pendo na hata wakafanikiwa mtoto wa kiume kwenye safari yao.

Hata hivyo, dunia iligeuka na kijana akamhepa na hivyo kuamua kuanika kila kitu kupitia mtandao wake wa Instagram.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke