Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Babake sajin Kenei adai DP Ruto amekimya kuhusu mauaji ya mwanawe

5d8ae6d69fe7afcf Babake sajin Kenei adai DP Ruto amekimya kuhusu mauaji ya mwanawe

Tue, 13 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Babake aliyekuwa mlinzi katika afisi ya DP Ruto Kipyegon Kenei amezunguza kwa mara ya kwanza kufuatia kifo cha mwanawe

- Kenei alipatikana akiwa ameuawa nyumbani kwake mtaani Imara Daima mwaka uliopita

- Uchunguzi wa awali ulionyesha kwamba Kenei alijitoa uhai, madai ambayo familia ilitupilia mbali

Familia ya Sajin Kipyegon Kenei imemshtumu Naibu Rais William Ruto kwa kutotimiza ahadi yake kufuatia mauaji ya mwana wao mwaka uliopita.

Inasemekana Ruto alipoitembelea familia ya Kenei,aliahidi kwamba angeisaidia lakini kufukia sasa haijasikia lolote kutoka kwa kigogo huyo.

Babake mwendazake marehemu Kenei amedokekezea kwamba huenda akafufua kesi ya mauaji kwa mwanawe endapo haki haitatendeka.

Kenei ambaye alikuwa mlinzi wa Ruto alipatikana akiwa ameuawa nyumbani kwake mtaani Imara Daima mwezi Februari mwaka jana.

Akihojiwa na runinga ya KTN Jumapili, Aprili 11, Joseph Chesang' alisema kwamba Ruto alitoa ahadi za uongo na sasa amemtaka ayatimize.

"Tangu wakati huo hakuna chochote kimetendeka na hatujawahi wasiliana. Tulitarajia kumuona kwa sababu alisema ni yeye alikuwa akilengwa na sio Kenei, hakuna chochote ambacho amefanya kufikia sasa," Alisema Chesang' akionekana kuwa mwingi wa mawazo.

Chesang bado anatilia shaka kwa matamshi ya naibu wa rais kwamba alimfahamu na hakujua Kenei ni mwanawe.

"Na kama angejua Kenei ni mtoto wangu ina maana angekuwa hai? Na kwa vile anajua hivyo kwa sasa kuna hatua gani amechukua? " Aliuliza kwa machungu.

Mzee Chesang alifichua kwamba kabla ya kifo chake kenei alilalamikia kunyanyaswa na wenzake huku hatua hake ya kuomba uhamisho ikigonga mwamba mara mbili.

"Mwanangu alitaka kuhamia kituo kingine kwasababu alikuwa Mtugen na wenzake walikuwa Wanandi, mshahara wake ulichelewa kwa mara nyingi na pia kuzuiwa kusafiri kwa mara nyingi." Chesang' aliongezea.

Chesang amepinga vikali madai kwamba mwanawe alijitoa uhai, alisisitiza kwamba aliuawa na watu maarufu serikalini.

"Wale walio uwa mwanangu wasiwahi pata amani, na wacha damu ya mwanangu iwafwate daima."

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke